Sunday, 9 March 2014

WABUNGE WALILIA MUDA

Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, wamependekeza kuongezwa  kwa muda wa uwasilishaji wa taarifa ya wachache kwenye kamati ya kujadili Rasimu ya Katiba na badala yake wachache wapewe muda zaidi ya nusu saa.
 
David Silinde, alisema kwa uzoefu wa Bunge la Jamhuri kundi la wachache huchukuliwa kama wapinzani na kupewa muda mchache ambao hautoshelezi kuwasilisha taarifa yao.
 
Alisema maoni ya wachache kwenye Bunge hilo si lazima yatokane na upinzani, bali kutoka kwenye makundi mbalimbali yanayounda Bunge hilo, hivyo ni vyema wakapewa muda wa dakika 50.
 
Mjumbe Lucas Malunde, alisema isijengeke dhana kuwa kundi la wengi ndilo lenye hoja za msingi na wachache wanaotoka upinzani hoja zao haina msingi, kuna muhimu wa kuongezewa muda na kuwasilisha taarifa yao na kujadiliwa.
 
Mjumbe Julius Mtatiro alisema dunia ya sasa ni demokrasia kwa wachache kupewa nafasi kwa kuwa wanaweza kuwa na mawazo mazuri kuliko walio wengi.
 
Mjumbe wa kamati ya Kanuni na Kumshauri Mwenyekiti, Evod Mmanda, alisema muda wa saa moja kwa taarifa ya wengi unatosheleza na nusu saa kwa wachache unatosheleza.
 
"Hisia zinajengeka kuwa hoja ya wachache unaweza kupigwa, kamati inaweza kuja na hoja ya wengi na ikapigwa vile vile," alisema.
 
Aidha, mjumbe Halima Mdee, alisema anashangazwa na uamuzi wa Mwenyekiti wa muda, Pandu Ameir Kificho, kuruhusu maboresho mengine kutoka kwa wajumbe na kusahau kuwa kifungu cha 33 kilishajadiliwa na kutolewa uamuzi wa saa moja kwa taarifa ya wengi na nusu saa kwa taarifa ya wachache.
 
Hata hivyo, Bunge hilo ilipitisha kanuni hiyo kwa maboresho ya taarifa ya wachache kusomwa kwa nusu saa na ya wengi kusomwa na Mwenyekiti wa kamati kwa saa moja.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments:

Post a Comment