Kwa karibu wiki sasa, hoja inayojadiliwa na
wajumbe wa Bunge hilo maalumu la katiba ni kanuni zitakazotumika
kuongoza chombo hicho.
Mjadala wa kuwepo kwa kura ya siri au ya wazi
katika kufanya uamuzi, umeonekana kuzua makundi mawili, moja
likijitanabaisha kama kundi la wazalendo na linalotetea masilahi ya
jamii huku jingine likitazamwa kuwa linatetea masilahi ya chama tawala.
Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa
nchini wanaona kuwa kuwapo kwa makundi yenye misimamo, hakuna madhara
katika mchakato unaoendelea.
Badala yake wanaeleza kuwa makundi hayo yamesababishwa na misimamo ya wale waliowatuma kuwawakilisha.
Wachambuzi hao wanasema kwa kuwa wajumbe wa Bunge
hilo wanayawakilisha makundi yenye mitazamo, mahitaji na mawazo tofauti
na ndiyo maana haishangazi kuona kutofautiana kwa mawazo na hata
kuonekana kuwepo kwa makundi yenye misimamo na mawazo tofauti.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk.
Alexander Makuliko anasema mvutano unaoonekana kuendelea mjini Dodoma ni
wa kawaida na uliotarajiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na ukweli kuwa
wajumbe hao ni wawakilishi wa makundi mbalimbali na yenye misimamo
tofauti katika jamii.
Anasema kutokana na ukweli huo, haishangazi
kukitokea kinachoonekana kuwa misimamo ya baadhi ya makundi kwa kuwa
misimamo ile ni maelekezo na makubaliano ya makundi wanayoyawakilisha.
“Hili la baadhi ya wajumbe kuonekana kutetea au
kuwa na misimamo ya makundi fulani ni la kawaida na lilitarajiwa
kabisa.Kumbuka kuwa makundi lazima yapeleke hoja zake, yavutane na lenye
hoja nzuri ndiyo lisikilizwa,” anasema.
Hata hivyo, Dk. Makulilo anapingana na dhana kuwa
masilahi ya taifa yawekwe mbele na kuhoji unawezaje kuyapima masilahi ya
taifa bila kuyaweka hayo makundi mbalimbali ya jamii?
“Kule kuna wawakilishi wa makundi mbalimbali, wapo
wawakilishi wa wavuvi, wakulima, wafugaji na wale wanaotoka katika
vyama vya siasa, yote haya ni makundi na kila moja lina masilahi
yake…hivyo, hakuna ubaya hata kidogo inapotokea kila moja likahakikisha
kuwa kundi lake linafaidika na katiba inayoandaliwa
Macho na masikio ya Watanzania kwa sasa yapo Dodoma ambako mjadala ya maandalizi ya mchakato wa kuandika Katiba Mpya.
Kwa karibu wiki sasa, hoja inayojadiliwa na
wajumbe wa Bunge hilo maalumu la katiba ni kanuni zitakazotumika
kuongoza chombo hicho.
Mjadala wa kuwepo kwa kura ya siri au ya wazi
katika kufanya uamuzi, umeonekana kuzua makundi mawili, moja
likijitanabaisha kama kundi la wazalendo na linalotetea masilahi ya
jamii huku jingine likitazamwa kuwa linatetea masilahi ya chama tawala.
Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa
nchini wanaona kuwa kuwapo kwa makundi yenye misimamo, hakuna madhara
katika mchakato unaoendelea.
Badala yake wanaeleza kuwa makundi hayo yamesababishwa na misimamo ya wale waliowatuma kuwawakilisha.
Wachambuzi hao wanasema kwa kuwa wajumbe wa Bunge
hilo wanayawakilisha makundi yenye mitazamo, mahitaji na mawazo tofauti
na ndiyo maana haishangazi kuona kutofautiana kwa mawazo na hata
kuonekana kuwepo kwa makundi yenye misimamo na mawazo tofauti.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk.
Alexander Makuliko anasema mvutano unaoonekana kuendelea mjini Dodoma ni
wa kawaida na uliotarajiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na ukweli kuwa
wajumbe hao ni wawakilishi wa makundi mbalimbali na yenye misimamo
tofauti katika jamii.
Anasema kutokana na ukweli huo, haishangazi
kukitokea kinachoonekana kuwa misimamo ya baadhi ya makundi kwa kuwa
misimamo ile ni maelekezo na makubaliano ya makundi wanayoyawakilisha.
“Hili la baadhi ya wajumbe kuonekana kutetea au
kuwa na misimamo ya makundi fulani ni la kawaida na lilitarajiwa
kabisa.Kumbuka kuwa makundi lazima yapeleke hoja zake, yavutane na lenye
hoja nzuri ndiyo lisikilizwa,” anasema.
Hata hivyo, Dk. Makulilo anapingana na dhana kuwa
masilahi ya taifa yawekwe mbele na kuhoji unawezaje kuyapima masilahi ya
taifa bila kuyaweka hayo makundi mbalimbali ya jamii?
“Kule kuna wawakilishi wa makundi mbalimbali, wapo
wawakilishi wa wavuvi, wakulima, wafugaji na wale wanaotoka katika
vyama vya siasa, yote haya ni makundi na kila moja lina masilahi
yake…hivyo, hakuna ubaya hata kidogo inapotokea kila moja likahakikisha
kuwa kundi lake linafaidika na katiba inayoandaliwa
{chanzo mwananchi}
{chanzo mwananchi}
No comments:
Post a Comment