Friday, 28 March 2014

BOCCO: UBINGWA NI WA AZAM

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco amewaambia wenzake kama wamedhamilia kutwaa ubingwa msimu huu ni lazima wahakikishe wanaishinda Simba Jumapili na Mbeya City.
Bocco aliiambia Mwananchi kuwa hakuna kingine zaidi ya kuwashinda wakongwe hao ili kuzidi kuwapoteza Yanga wanaokabana nao  jino kwa jino katika mbio hizo za ubingwa.
Mshambuliaji huyo alisema hawana budi kukomaa na kuhakikisha wanashinda mechi hizo ili kuzidi kufufua matumaini yao ya kupata ubingwa kwa mara ya kwanza msimu huu.
Alisema mechi walizobakiwa nazo ni ngumu ingawa wengi wanaona kuwa watapata vikwazo zaidi katika mechi dhidi ya Simba na Mbeya City hivyo wanataka kuwadhihirishia watu kuwa wamejipanga na watavuka vikwazo vyote hivyo wanavyofikiria.
“Lengo letu msimu huu ni kutwaa ubingwa na ndio maana tumejipanga na hatutaki kupoteza mchezo wowote, lakini muhimu kwanza ni kukivuka hiki kigingi dhidi ya Simba Jumapili, iwe isiwe lazima tujitahidi.
“Sasa hivi hatupaswi kupoteza mchezo wowote kwani tukiteleza tu wapinzani wetu watachukua nafasi, maana hali ilivyo tunakwenda kila mmoja anamuombea mwenzake apoteze ndio maana nawaomba wenzangu tujitahidi tukomae mpaka mwisho,” alisema Bocco.

<MWANANCHI>

No comments:

Post a Comment