Thursday, 6 March 2014

OKWI , NGASA NA KIIZA WAMEKUWA TISHIO MISRI

Dar es Salaam. Kocha wa Mabingwa wa Soka Afrika, Al Ahly, Mohamed Youssef amesema kati ya wachezaji anaowatilia shaka na ana hofu nao katika mechi ya marudiano Jumapili itakayochezwa saa mbili kamili kwa saa za hapa nchini ni Mrisho Ngasa, Hamis Kiiza na Didier Kavumbagu.
Youssef alikaririwa na mtandao wa mmoja wa Misri, akisema kuwa wachezaji hao ni tishio kwake kwa mchezo huo, lakini akamtaja mshambuliaji mwingine, Emmanuel Okwi kuwa ni kati ya wachezaji hatari kwa ngome yake.
“Kutokana na wachezaji wetu kuwa majeruhi, imesababisha kushindwa mechi tatu zikiwemo za ligi,” alisema Youssef na kudai kuwa wachezaji wake watakuwa na kazi ya kumchunga, Mrisho Ngasa ambaye alionyesha soka ya kiwango cha juu.
Ngasa, ambaye hakufanya vizuri kwenye majaribio yake 2009 katika klabu ya England ya West Ham, alifunga mabao matatu katika kila mechi dhidi ya Komorizone katika mechi za hatua ya awali.
Yanga ilipambana na Al Ahly katika mchezo wa kwanza wa raundi ya kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita na Yanga kushinda bao 1-0 lililofungwa na Nadir Haroub ‘Canavaro’ baada ya kuunganisha mpira wa kona uliompita kipa wa Al Ahly, Sherif Ekrami na kujaa wavuni.
Tayari Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limeandika barua Fifa kuomba maelekezo iwapo mashabiki wa Yanga wataruhusiwa kushuhudia pambano hilo ambalo Yanga inatakiwa kucheza kufa aukupona kuhakikisha inatoka na ushindi ili iweze kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
“Wasiwasi wetu Fifa isije ikairuhusu Yanga ikajikuta haina mashabiki, tunategemea mpaka leo jioni (jana) tutakuwa tumeshafahamu msimamo wa Fifa kama wanaruhusu mashabiki wa Yanga nao waende, na pia wasije wakaenda wakajikuta wanabaki nje ya uwanja,” alisema Wambura. {chanzo mwananchi}

No comments:

Post a Comment