Mwaka 1972, Mwalimu Julius Nyerere akiwa rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, alitangaza Azimio la Iringa lililokuwa na kauli
mbiu ya ‘Siasa ni Kilimo.’
Ilikuwa ni baada ya kufafanua falsafa ya maendeleo
kwamba ili tuendelee tuna hitaji vitu vinne – watu, ardhi, siasa safi
na uongozi bora.
Tafsiri ya maneno haya ni kwamba nguvu kazi na ardhi ni muhimu katika maendeleo ya kilimo nchini.
Hadi sasa sekta ya kilimo inayokua kwa asilimia nne, imeajiri asilimia 75 ya Watanzania, wengi wao wakiwa ni wakulima wadogo.
Serikali katika awamu zake tatu zilizotangulia
ilijitahidi kuhamasisha kilimo kwa kuwaandaa wataalamu na kutumia
wanasiasa katika majukwaa yao ili kuhimiza kilimo ambacho mpaka sasa
hakina mafanikio ya kuridhisha.
Hivi karibuni kulikuwa na maadhimisho ya mwaka wa
kilimo kwa Afrika, uliofanikishwa na Jukwaa la Kilimo (Ansaf) naTaasisi
ya One ya Afrika Kusini, uliofanyika Kijiji cha Kaning’ombe wilayani
Iringa, Mkoa wa Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma
aliyemwakilisha Makamu wa Rais, Dk. Gharib Bilal, alikutana na
kuzungumza na wakulima.
Mkulima wa mfano
Mkulima Eusebio Mbangile alipewa nafasi ya
kuonyesha shamba lake kwa Dk. Ishengoma hivyo kuwa mfano wa utekelezaji
wa Azimio la Siasa ni Kilimo.
Baada ya kusota na kilimo kisichokuwa na tija kwa
muda mrefu, Mbangile ameibukia kuwa mkulima mwenye mafanikio baada ya
kufuata ushauri wa kitaalamu akiwa na shamba la ekari 46 ambalo amepanda
mahindi na miche ya matunda.
Mbangile anasema shamba lake ameligawa katika
vitalu vitatu na kitalu cha kwanza amepanda mahindi ambayo anatazamia
kupata magunia 25 kwa ekari moja.
“Eneo hili la pili lina ukubwa ekari nane ambalo
analima bila kuweka mbolea ya kukuzia. Natarajia kupata gunia 15 hadi 16
kwa ekari moja.Nikiweka tofauti ya eneo la kwanza na la pili, naona
hapa mazao yanapungua,” anasema Mbangile. Eneo la tatu ambalo lina ekari
3.5, mkulima huyo ametumia Sh1.7 milioni kuandaa shamba hilo.{CHANZO MWANANCHI}
No comments:
Post a Comment