Thursday, 13 March 2014

LIGI DARAJA LA KWANZA HAPASHIKIKI



Dar es Salaam. Wakati Polisi Morogoro ikiwa ya kwanza kupanda Ligi Kuu msimu wa 2014/2015, timu nyingine tano za ligi daraja la kwanza zinachuana kuwania nafasi mbili zilizobakia.
Timu hizo ni Kanembwa JKT, Mwadui na Stendi United ambazo zinachuana kusaka nafasi moja ya kucheza Kigi Kuu kwenye kundi C, ambapo kila moja ina pointi 19 na mechi nne mkononi.
Katika kundi A, timu ya African Lyon iliyoshuka daraja msimu uliopita inachuana vikali na Ndanda kuwania nafasi moja katika kundi A ya kucheza Ligi Kuu msimu ujao.
Kwa mujibu wa ofisa wa bodi ya ligi (TPLB), Joel Balisidya, Lyon inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 23 ikifuatiwa na Ndanda yenye pointi 22 huku kila moja ikibakiwa na michezo miwili. “Kundi B tayari Polisi Morogoro imepanda kucheza Ligi Kuu ikiwa na pointi 25 na mechi mbili mkononi ambazo timu nyingine za kundi lake haiwezi kuzifikisha,” alisema Balisidya.
Katika kundi hilo la B, Mlale JKT ina pointi 17 sawa na Bukina Faso na Lipuli huku kila moja ikiwa na michezo miwili ambayo hata zikishinda michezo yote zitafikisha pointi 23 kila moja.
Kwenye kundi C, Toto African ina wakati mgumu wa kupanda Ligi Kuu mbele ya Kanembwa JKT, Mwadui na Stendi United ambazo zinachuana kutafuta tiketi hiyo moja.
Chanzo mwananchili

No comments:

Post a Comment