Monday, 31 March 2014

MAFURIKO YAUA NA KUSITISHA USAFIRI


DSC_0413DARAJA la MTAMA Llilokatika Tarehe 26/3/2014 na kuzuia mawasiliano ya barabara kati ya lindi na newala kwenda Tandahimba mkoani Mtwara.DSC_0367Baadhi ya abiria walionasa kufuatia kukatika kwa daraja Nyangao wilayani Lindi kutokana na Mvua zinazoendelea
DSC_0377Kamati ya Ulinzi na Usalama ilkiongozwa na mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa wa Lind, Ludovick Mwananzila ilipofika eneo la Nyangao kukagua athari za Mafuriko hayo.DSC_0103Mmoja wa abiria aliekwama baada ya kukatika kwa daraja la Nyangao linalounganisha barabara ya lindi na masasi kwenda Nachingwea na Tunduru akijaribu kuvuka mara baada ya kutengeneza njia ya muda kunusuru abiria kutokana na mafuriko yaliyotokea Tarehe 26/3/2014.DSC_0198Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila akiithibitisha njia ya muda mara baada ya kukatika kwa daraja la mto Nyangao lililokatika jana, Kulia ni Kamanda wa polisi mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga waliofika kukagua athari zilizojitokezaDSC_0316Baadhi ya abiria wakivuka katika daraja la Nyangao Lindi picha na Abdulaziz Lindi

Na. Abdulaziz Video, Lindi
 
Mafuriko yaua na kusitisha usafiri Lindi Masasi,Ruangwa na Nachingwea ikiwemo Newala na Tandahimba Mkoani Mtwara
 
Watu Wanne wamefariki dunia katika wilaya ya Lindi kutokana na mvua zilizonyesha usiku wa Tarehe 26 na 27 /3/2014 na kusababisha mafuriko makubwa katika maeneo mbalimbali ya wilaya za Lindi, Nachingwea na Ruangwa Mkoani Lindi

Sambamba na mvua hizo licha ya kupoteza maisha ya watu hao na wengine kujeruhiwa pia Imesitisha huduma za usafiri kati ya Lindi, Masasi, Nachingwea, Ruangwa na Newala kufuatia kukatika kwa madaraja ya Mtama na Nyangao pamoja na makazi ya wananchi wanaoishi pembezoni kulikosababishwa na kufurika kwa mto Lukuledi.
 
Akiongea na globu hii mara baada ya kukagua athari hizo, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila alieleza kuwa Tayari Wakala wa barabara Mkoa wa Lindi inafanya jitihada za haraka kuweka njia ya Muda ili kuokoa wananchi wengi waliokwama katika maeneo hayo ili kupunguza msongamano uliopo Sambamba hilo Mwananzila alitoa wito kwa baadhi ya wananchi waliopo maeneo yaliyokumbwa na maafa hayo kutoruhusu watoto wao kucheza katika mto huo kutokana na ongezeko kubwa la maji.
 
Aidha Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi aliwahakikishia usalama abiria wote waliokutwa na maafa hayo kuwa Jeshi la polisi limejipanga kutoa ulinzi wakati wote katika maeneo hayo huku akitoa agizo kwa wenye mabasi ya Abiria kutofanya safari hadi kutakapokamilika kwa maeneo hayo ili kupunguza idadi kubwa ya wasafiri.
 
Kukatika kwa madaraja hayo tayari kumesitisha Usafiri kwa wanaotoka Mkoa wa Lindi kwenda wilaya za Masasi, Nachingwea, Tunduru, Ruangwa, Liwale, Nanyumbu, Newala  

<HABARI KWANZA>

Friday, 28 March 2014

BOCCO: UBINGWA NI WA AZAM

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco amewaambia wenzake kama wamedhamilia kutwaa ubingwa msimu huu ni lazima wahakikishe wanaishinda Simba Jumapili na Mbeya City.
Bocco aliiambia Mwananchi kuwa hakuna kingine zaidi ya kuwashinda wakongwe hao ili kuzidi kuwapoteza Yanga wanaokabana nao  jino kwa jino katika mbio hizo za ubingwa.
Mshambuliaji huyo alisema hawana budi kukomaa na kuhakikisha wanashinda mechi hizo ili kuzidi kufufua matumaini yao ya kupata ubingwa kwa mara ya kwanza msimu huu.
Alisema mechi walizobakiwa nazo ni ngumu ingawa wengi wanaona kuwa watapata vikwazo zaidi katika mechi dhidi ya Simba na Mbeya City hivyo wanataka kuwadhihirishia watu kuwa wamejipanga na watavuka vikwazo vyote hivyo wanavyofikiria.
“Lengo letu msimu huu ni kutwaa ubingwa na ndio maana tumejipanga na hatutaki kupoteza mchezo wowote, lakini muhimu kwanza ni kukivuka hiki kigingi dhidi ya Simba Jumapili, iwe isiwe lazima tujitahidi.
“Sasa hivi hatupaswi kupoteza mchezo wowote kwani tukiteleza tu wapinzani wetu watachukua nafasi, maana hali ilivyo tunakwenda kila mmoja anamuombea mwenzake apoteze ndio maana nawaomba wenzangu tujitahidi tukomae mpaka mwisho,” alisema Bocco.

<MWANANCHI>

NGOLOLO YAMPONZA DIAMOND MAULIDINI

KIJOGOO wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewachefua waumini wenzake wa Kiislamu baada ya kutupia swaga za staili ya Ngololo kwenye shughuli ya Maulidi.
Kijogoo wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz akicheza staili ya Ngololo kwenye kaswida.
Tukio hilo lililowagusa waumini hao lilitokea juzikati ambapo kulifanyika Maulidi ya kumtoa nje mtoto wa dansa wake aitwaye Moze Lyobo maeneo ya Mbagala, jijini Dar.
Awali watu waliokuwepo eneo hilo walifurahia uwepo wake lakini kadiri walivyoaanza kugundua kasoro ndipo mambo yalipoanza kuharibika.
Diamond akiwa kwenye shughuli hiyo.
“Watu hawakumshtukia, lakini walipomkagua kwa makini na kugundua licha ya kuvaa mavazi ya
Kiislamu ndani yake ana macheni ya dhahabu shingoni kitu ambacho dini hairuhusu,” kilidai
chanzo baada ya mwandishi wetu kufika eneo la tukio na kukuta shughuli imeisha.
Kama hiyo haitoshi, ikaelezwa kuwa Diamond alizidi kuchafua hali ya hewa baada ya kucheza
staili ya Ngololo kwenye kaswida kitu ambacho kiliwashangaza wengi.
...Diamond akiwa na mtoto wa Moze Lyobo aliyefanyiwa Maulidi.
“Mwanzo alianza vizuri lakini kadiri dufu lilivyokuwa linakolea, akawa anajisahau na kucheza
Ngololo, kimsingi aliwaboa baadhi ya Waislamu waliokuwa pale,” alisema shuhuda wetu.
Hata hivyo paparazi wetu alitonywa kuwa, baada ya kucheza sana, Diamond alichoka huku jasho
likimchuruzika ambapo aliamua kupumzika na kuwaacha wengine wakiendelea.

chanzo GPL

HARUFU YA RUSHWA BUNGE LA KATIBA


SHARE THIS STORY
0
Share


Dar es Salaam. Hali ya hewa jana ilichafuka kwenye Bunge la Katiba baada ya mjumbe Ezekiel Wenje kuwatuhumu Waziri Mkuu Mizengo Pinda na baadhi ya mawaziri kuwa waliwahonga baadhi ya wajumbe wa kundi la 201.
Katika tuhuma hizo, Wenje alimtaja Waziri Profesa Jumanne Maghembe, Dk. Shukuru Kawambwa na Gaudensia Kabaka akisema kuwa walitoa rushwa ya vyakula, maji na vinywaji kwa wajumbe hao ili waunge mkono msimamo wa serikali mbili.
Kauli hiyo, iliyotolewa katika mjadala wa mabadiliko ya kanuni, ilisababisha mawaziri hao kunyanyuka kujibu tuhuma hizo, huku Wenje akisisitiza kuwa aliyoyasema ni kweli tupu.
Vilevile baadhi ya wajumbe wanaotoka katika kundi hilo walicharuka na kujaribu kujitetea huku mmojawapo akitishia kuwa iwapo Wenje asingeomba radhi, asingetoka ndani ya Bunge hilo.
Hoja ilipoanzia
Wenje, ambaye pia ni mbunge wa Nyamagana (Chadema), alianza kwa kueleza kwamba wapinzani “walilia” sana kuwa Bunge la Katiba lisingekuwa na usawa kutokana na Chama cha Mapinduzi kuwa na wajumbe wengi, ndipo ikaonekana wapatikane wajumbe wengine 201, lakini jambo la ajabu ni kwamba walioteuliwa katika kundi hilo asilimia 80 ni makada wa CCM akiwamo mzee maarufu ambaye ameingizwa kama mganga wa jadi.
Ingawa hakumtaja jina, Wenje alikuwa anamaanisha kada mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale-Mwiru aliyeteuliwa kupitia kundi la waganga wa jadi.
Kuhusu rushwa, Wenje alisema:“…Sasa kuna wajumbe wa kundi la 201 walipelekwa kwa Profesa Maghembe na Dk. Kawambwa wamepeana rushwa, vikao vingi vilifanyika usiku. Hii haikubaliki.”
Baada ya kauli hiyo ya Wenje, Profesa Maghembe alisimama ghafla huku akionekana kutaharuki, ambapo Makamu Mwenyekiti Samia Suluhu Hassan alimpa nafasi ya kujieleza.
Profesa Maghembe alikiri kuwakaribisha baadhi ya wajumbe wa kundi hilo, akieleza kwamba ilikuwa ni katika hali ya ukarimu uliozoeleka miongoni mwa jamii ya Kitanzania.
“Kuna kundi lipo hapa ambalo linafanya kazi ya kudhalilisha wenzao. Ni kweli niliwaalika kwa chakula wajumbe hao kwa taratibu za kawaida, lakini hakuna mbunge hapa anayeshindwa kujinunulia chakula, hakuna anayeweza kupewa rushwa.
“Kwa sababu hiyo ninaomba kiti chako kimtake mjumbe aliyewasilisha hoja hiyo aniombe radhi. Wenje aniombe radhi,” alisema Profesa Maghembe akiwa katika hali ya hasira, huku kukiwa na sauti za kuzomea na kushangilia kutoka kwa wajumbe.

<mwananchi>

MVUA YAWATESA WAKAZI WA JANGWAI DAR ES SALAAM


Hivi ndivyo maji yanavyo onekana kujaa katika makazi Jangwani
Baadhi ya watu wakionekana nje baada ya maji kuingia ndani.

Muonekano wa nyumba pamoja na njia ndogo ndogo zikiwa zimejaa maji.
Picha na Husein wa Dar es salaam yetu Blog
chanzo GPL

Thursday, 27 March 2014

TATIZO LA KOTOKWA NA DAMU UKENI

Tatizo hili huwasumbua wanawake wengi walio katika umri wa kuzaa na baadhi ya wanawake ambao tayari wameshafikia ukomo wa kuzaa.
Kwa mwanamke aliyekwishafunga kupata hedhi kuendelea kupata damu ya hedhi au kutokwa na damu ukeni bila ya mpangilio siyo hali ya kawaida.
Mwanamke anaanza kuvunja ungo kuanzia umri wa miaka 12 na hufikia ukomo kuanzia umri wa miaka 45. Kupatwa na damu ukeni chini ya umri wa miaka 40 kuna vyanzo vingi kama tutakavyoona.
Chanzo cha tatizo
Damu kutoka bila ya mpangilio kwa mwanamke ambaye hajakoma hedhi husababishwa na mabadiliko katika mfumo wa homoni endapo hazipo sawa ‘Hormonal Imalance.’ Uwepo wa uvimbe katika kizazi na matumizi ya dawa za homoni mfano sindano au vipandikizi. Kuweka kitanzi katika kizazi pia huwafanya wanawake wengine wapate hali hii ya kutokwa na damu bila mpangilio.
Mabadiliko ya mfumo wa homoni huweza pia kusababishwa na mshtuko wa mwili au hali ya mabadiliko ya mazingira.
Kuharibika kwa mimba pia ni mojawapo ya sababu kubwa. Mwanamke mwenye umri wa zaidi ya miaka 45 kupata damu ukeni bila ya mpangilio ni vema kuchunguza kwa undani kwani wana uwezekano mkubwa wa kuwa na saratani ya kizazi au shingo ya uzazi.
Dalili za tatizo
Mwanamke hulalamika kuona siku za hedhi zaidi kuliko kawaida yake, au kuona katikati ya mzunguko yaani aliona, ikaacha sasa inaanza tena.
Damu inaweza kuwa nyingi na mwanamke akabadilisha pedi mara nyingi kuliko kawaida  yake au akapata kidogokidogo lakini kwa muda mrefu.
Damu inaweza kuwa nyepesi au nyeusi au nzito na mabonge. Hutoa harufu isiyo ya kawaida endapo ata-bleed kwa muda mrefu.
Ikiwa na mabonge huambatana na maumivu.
Mgonjwa huchukua muda mrefu hata zaidi ya majuma mawili akiwa anatokwa na damu, endapo hatapata tiba haraka huanza kuumwa tumbo chini ya kitovu ikiwa ni dalili za kupatwa na maambukizi ya kizazi kwa kuwa bakteria hupenda sana mazingira ya damu.
Hali inapoendelea mwanamke hupoteza uwezo wa kushika mimba na huathiri uzazi kwani hushindwa kufanya tendo la ndoa, homoni zinavurugika na maambukizi ya kizazi huathiri mirija ya mayai.
Uvimbe wa Fibroid ukiwa ndani ya kizazi husababisha damu zitoke bila ya mpangilio na kuzuia mimba kukua na hata ikiingia inaweza isiendelee.
Uchunguzi
Tatizo hili ni sugu na huleta athari kubwa katika mfumo wa uzazi wa mwanamke hivyo ni vema uchunguzi wa kina ukafanyika katika hospitali kubwa. Vipimo vya damu kuangalia mfumo wa homoni, kipimo cha Ultrasound kuangalia kizazi na vifuko vya mayai pia hufanyika.
Ushauri
Usidharau tatizo hili la kutokwa na damu bila mpangilio ukeni ukiwa bado binti au mtu mzima kwani madhara yake ni makubwa. Muone haraka daktari kwa uchunguzi na tiba.

chanzo GL

PESA ZA MKONGO ZAWACHANGAYA WOLPER NA HUSNA

Mambo hadharani! Kigogo ambaye ni raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo anayewagombanisha mastaa wawili Bongo, Jacqueline Wolper Massawe na Husna Maulid ni huyu hapa.
Staa wa Bongo Muvi, Jacqueline Wolper Masswe.
Anaitwa Rajab Mwami Shamweshi.
Habari zilizolifikia Ijumaa zilidai kwamba baada ya mtafaruku wa mastaa hao kuripotiwa na gazeti mama la hili, Uwazi la Jumanne iliyopita, jamaa huyo aliibuka na kuanza kulalamika kwa watu wake wa karibu kuwa anachafuliwa mitandaoni kwa sababu ya mastaa hao.
Patchou Mwamba ‘Tajiri’.
PATCHOU MWAMBA NDANI
Ilidaiwa kuwa Mwami alichukizwa na ishu hiyo kwani ilimhusisha mwanamuziki wa FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ ambaye pia ni mwigizaji, Patchou Mwamba ‘Tajiri’ kuwa ndiye humkuwadia kwa mastaa.
TUANZE NA PATCHOU
Kabla ya kumpata Mwami mwenyewe, Ijumaa lilizungumza na Patchou uso kwa uso amba alifunguka anachokijua juu ya sakata la Wolper na Husna kumgombea mwanaume huyo.
Alisema: “Mimi nashangaa kuona nachafuliwa mitandaoni lakini ukweli anayefanya hivyo ni Husna.
“Huyo Husna ni kweli aliwahi kutoka na Mwami lakini baadaye alimdharau Mwami kwa sababu alimuona hana pesa.
Mlimbwende Husna Maulid.
“Baada ya kuona pesa zimemtembelea Mwami akataka kurudi ndipo akakuta jamaa ameshajiweka kwa Wolper. Hapo ndipo Husna akaanza kuchanganyikiwa.” Patchou aliendelea kuweka wazi kwamba yeye na Mwami ni mtu na rafiki yake na pia ni ‘mapatna’ kwenye biashara.
Alisema amekuwa akikutana naye mara kwa mara Nairobi, Kenya na ndiye aliyemleta Bongo kwa ajili ya kuanzisha kampuni ya michezo ambapo alifikia hotelini.
KUWADI?
Alitiririka kwamba hajawahi kumkuwadia mwanamke lakini anachojua Mwami ni anajuana vizuri na
Wolper kwani alimtambulisha walipokutana Nairobi hivi karibuni ndipo akaujua uhusiano wao.
Patchou: “Nilishangaa kwa sababu baada ya Mwami kutua tu Bongo, wasichana wa mjini walipojua
ndipo wakaanza kumsaka hadi chumba alichofikia hotelini.“Wengine walidiriki hata kumtumia picha za utupu ili kuwa naye kimapenzi baada ya kupata namba yake.”
Patchou alisisitiza kuwa yeye si kuwadi kama wanavyomtangaza kwani hata huyo Wolper alishtukia amekutana naye Nairobi wakiwa na Mwami kwani kabla ya hapo alikuwa hajuichochote.
Baada ya kumaliza kutoa utetezi wake, aliombwa kumpigia simu Mwami na kumuweka loud speaker
(sauti ya juu) ambapo alimweleza Mwami kila kitu ndipo akakubali kuzungumza na wanahabari wetu akiwa London, Uingereza.
KIGOGO AFUNGUKA
Akizungumzia sakata hilo, Mwami ambaye anadaiwa kuwa na ‘mihela’ hivyo kujitwalia taito ya ukigogo alisema kuwa anamfahamu Husna kama mtu wa kawaida ambaye aliwahi kufahamiana naye.
KUHUSU WOLPER
Kwa upande wa Wolper alisema kuwa anamfahamu kwa kumsikia na kumuona lakini si kimapenzi kama wanavyomchafulia jina.
“Nilipokuja Tanzania kwa mara ya kwanza nilifikia hotelini…(anaitaja), kama wanavyodai hata chumba ndicho chenyewe lakini sikuja kwa ajili ya starehe za kimapenzi na wanawake, nilikuja kwa biashara zangu, nashangaa kuona nawekwa mitandaoni hovyo na anayeniweka namfahamu.
“Naomba nisizungumze sana, niishie hapo nikirudi Tanzania nitaongea nanyi kwa uwazi kabisa,” alisema Mwami.
FUMANIZI
Wolper na Husna ambao waliwahi kuwa mashosti walianza manenomaneno hivi karibuni ambapo awali haikujulikana chanzo hadi pale Husna alipoamua kulifungukia hilo la mwanaume.
Ijumaa lilifanya jitihada za kumsaka Wolper kupitia simu yake ya mkononi, alipopatikana alisema angefika ofisini kwetu kutoa ufafanuzi lakini mpaka gazeti linakwenda mtamboni alikuwa hajafika na alipotumiwa sms ya kuulizwa kama angefika au la hakujibu

.chanzo gpl

MAAJABU YA DUNIA MCHUNGAJI AZIKWA KIISLAMU

Maajabu! Mchungaji wa Kanisa la Pentecostal Spirit and Truth, Amani Rubeni Mirumbe ameushangaza ulimwengu kwa kujitabiria kifo na baadaye kufariki dunia kweli huku akiwaachia waumini na familia yake wosia wenye viashiria vya kuzikwa Kiislam, Amani linakujuza.
Mwili wa mchungaji Amani Rubeni Mirumbe ukiagwa.
Kifo hicho kilijiri saa 3:12 asubuhi ya Machi 24, mwaka huu, Mabibo jijini Dar es Salaam mahali lilipo kanisa na nyumba ya mchungaji huyo na kuzikwa saa 10:21 jioni. Kwa maana hiyo, mwili huo ulikaa kwa saa saba tu.
KILICHOSABABISHA KIFO
Saa chache baada ya kifo, Amani lilifika msibani na kufanikiwa kubaini mawili matatu kuhusu kifo cha mtumishi huyo wa Mungu.
Kwa mujibu wa mmoja wa waumini wake, marehemu Mchungaji Mirumbe alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya presha lakini asubuhi ya siku ya tukio, alipoamka alimwita msaidizi wake na kumwambia siku hiyo haiwezi kupita bila yeye kukata roho.
“Ni ajabu sana, alipoamka tu alimwita msaidizi wake, akamwambia siku ya leo (Jumatatu) lazima afe ila kabla ya kuiacha dunia anataka kuacha wosia wake kwa ajili ya familia na sisi waumini,” alisema muumini mmoja ambaye aliomba hifadhi ya jina.
WOSIA NI HUU
Muumini huyo alisema kuwa, mchungaji huyo akiwa katika hatua za mwishomwisho kabla ya kifo, aliacha wosia kwamba, akishakata roho hatataka mwili wake uzikwe ukiwa ndani ya jeneza kama wafanyanyiwavyo Wakristo au wachungaji wengine.
Ndugu wa mchungaji Amani Rubeni Mirumbe wakiomboleza kwa simanzi kubwa
“Marehemu aliagiza mwili wake uwekwe kwenye sanda na hata kama ataagwa zoezi hilo lifanyike mwili ukiwa ndani ya sanda ambayo itazungushiwa mkeka,” muumini huyo alizidi kuanika wosia huo.
KUHUSU MAITI YAKE
Katika wosia huo, Mchungaji Mirumbe aliagiza maiti yake isilale hata usiku mmoja na wala isisafirishwe kwenda kwao mkoani Mara kwa mazishi.“Alisema akitokea mtu kimbelembele na kujiamulia kuisafirisha maiti yake kwenda kuzikwa kokote nje ya Dar, basi ajue atarudi nayo atake asitake,” kilisema chanzo.

HAKUNA KULIA
Mwisho marehemu huyo hakutaka waumini wake wale familia yake kumwaga machozi kufuatia kifo chake kama njia ya kuomboleza.
WAUMINiWAUPOKEA MWILI
Amani liliwashuhudia waumini wa kanisa hilo wakiupokea mwili wa mchungaji wao kutoka ndani ya nyumba yake ulikokuwa umehifadhiwa baada ya kifo ukiwa umeviringishwa kwenye mkeka na kupelekwa kanisani kwa ajili ya kuombewa na kuagwa kabla ya kupelekwa makaburini.
Wakati wa kuuaga mwili, baadhi ya ndugu na waumini wachache walionekana kuvunja wosia wa mchungaji huyo ambapo walionesha wazi masikitiko yao kwa kuangua vilio licha ya kuonywa na baadhi ya viongozi.
HALI YA MAKABURINI
Mwili huo ukiwa ndani ya sanda iliyozungukwa na mkeka uliwekwa juu ya meza ndani ya kanisa lake. Baada ya zoezi hilo, ndugu na waumini waliuchukua mwili huo hadi kwenye Makaburi ya Ubungo Fishnet Industry ‘Ufi’, Shekilango jijini Dar kwa mazishi ambapo mwili uliingizwa kwenye mwanandani.
Baadhi ya ndugu na waumini walisimamia wosia kuhakikisha hakuna kisichofuatwa ambapo walisimamia zoezi la kumzika mchungaji huyo pasipo kitu chochote zaidi ya sanda tu kama alivyoagiza.
Mwili wa mchungaji Amani Rubeni Mirumbe ukizikwa.
MTOTO WA MAREHEMU ANENA
Akizungumza na mwandishi wetu makaburini hapo, mtoto wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Adam Mirumbe alithibitisha utabiri wa kifo na wosia wa baba yake kwa msikitiko.
“Kweli baba aliniambia kuwa angekufa leo na alinipa wosia kuwa maiti yake isilale, isisafirishwe, watu wasilie msibani na kubwa zaidi ni kwamba azikwe bila jeneza, yaani na sanda tu kama ulivyoona. Unaweza kusema amezikwa Kiislam, lakini yeye aliamini atakuwa amezikwa kama Yesu,” alisema mtoto huyo.

KUHUSU MKE WA MAREHEMU
Adam aliongeza kuwa, wakati kifo cha baba yake kinatokea, mama yake hakuweza kuhudhuria kwa sababu alikuwa safarini kuelekea Musoma, Mara kwenye msiba wa mtoto mwingine ambapo maziko yake ilibidi yasimamishwe mpaka mwili wa mchungaji huyo uhifadhiwe kwenye nyumba yake ya milele.
Ndugu na jamaa wa mchungaji Amani Rubeni Mirumbe wakiwa kwenye maziko.
KUMBE NI BABA WA MSANII WA BONGO MUVI
Mwandishi wetu aliwashuhudia wasanii wa filamu Bongo ‘Bongo Movies’, Mohammed Mwikongi ‘Frank’ na Michael Philip ‘Kojaki’ wakimtia nguvu msanii mwenzao ambaye ni mtoto mmojawapo wa mchungaji huyo ambaye kisanii anajulikana kwa jina la Mgomakufa.

KWA  NINI KIISLAM?
Baadhi ya watu waliohudhuria msiba huo walishindilia utaratibu huo kuwa ni wa imani ya Kiislam wakidai kwamba, mwili huwa haulali (labda dharura), hauzikwi ukiwa ndani ya jeneza (sanduku) na huwekwa kwenye mwanandani.
“Sijui kwa nini mchungaji aliamua kutoa wosia huo? Huenda kuna kitu alikiona ambacho kilimpa ishara kwamba, kuzikwa ndani ya jeneza na maiti yake kulala kuna mambo atayakosa mbele ya safari akhera,” alisema mwombolezaji mmoja.
MAZISHI YA KIKRISTO
Katika utaratibu wa mazishi ya Kikristo, mwili huhifadhiwa ndani ya jeneza, unaweza kulala hata siku tatu bila kuzikwa, hakuna mwanandani kwa sababu mwili unakuwa ndani ya sanduku.

chanzo GPL

AUNGUA SEHEMU ZAKE ZA SIRI

KATIKA tukio linalohusishwa na ushirikina, mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Doto Omari (30, pichani) ameunguzwa na moto wa ajabu sehemu zake za siri.
Moja ya jeraha alilolipata.
Tukio hilo la aina yake lilitokea alfajiri ya Machi 16 mwaka huu,   Mwananyamala – Kichangani, Dar,  wakati mwanamke huyo alipokwenda chooni kujisaidia.
Akizungumza na waandishi wetu, Doto alisema alipoanza kujisaidia, alishangaa kuona moto mkubwa ukitokea ndani ya shimo la choo na kumuunguza sehemu zake za siri, jambo lililomfanya apige kelele kuomba msaada.
“Yaani ule moto ulikuwa mkubwa halafu wa kijani huku ukiwa na muungurumo wa ajabu. Mimi nilishangaa kuuona ukinifuata na kuniunguza,” alisema.
Kaka wa mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina la Adam, alisema aliposikia kelele za moto, alikimbilia maji akijua ni wa kawaida.
“Mpaka sasa tumechanganyikiwa sana, hilo siyo tukio la kwanza, yako mengi, nilishawahi kumuona mtu wa ajabu  kainama kwenye mlango wa kuingilia chooni halafu kufumba na kufumbua akapotea, hii nyumba siyo kabisa.
 “Wengi ukiwaambia jambo hili huona kama hadithi, lakini matukio ya aina hii hapa Kichangani ni jambo la kawaida sema watu wanaogopa kusema,” alisema Adam.AUo zaidi ya kumuona wifiye akigaragara chini akidai kuungua.
Hadi waandishi wetu wanaondoka eneo la tukio, ndugu hao walikuwa wakijiandaa kumpeleka Doto kwa mganga wa kienyeji maeneo ya Lugoba, Chalinze kwa matibabu

chanzo GPL

DOGO JANJA SHULE NDIO MAFANIKIO


Abdulaziz Chende 'Dogo Janja' kutoka Ngarenaro.
ABDULAZIZ Chende ndilo jina lake halisi alilokuja nalo jijini Dar es Salaam akitokea Ngarenaro, kule mjini Arusha, lakini wajanja wa mjini wakambatiza kama Dogo Janja, ambalo kwa kweli limemkaa vyema.
Ni bwana mdogo kweli, siyo tu kwa umri, bali hata sanaa aliyoichagua. Ni kijana ambaye kwa jinsi watoto wa Dot.com walivyo, alistahili kuwa kidato cha kwanza, pili au hata cha tatu. Ulimwengu wa Bongo Fleva, ulimtambua baada ya kutambulishwa na Kundi la Tip Top Connection, kupitia kwa kinara wake, Madee.
Dogo janja akiwa mzigoni.
Dogo anaweza kurap. Lafudhi yake ya watoto wa Kiarusha inamuongezea ‘credit’ katika muziki wake, kwa sababu nayo ni kitambulisho kingine cha uwepo wake. Wakati akitambulishwa, Madee aliwaahidi mashabiki kuwa atamlea Dogo katika njia inayofaa, ikiwa ni pamoja na kumkuza kisanii na kielimu.
Simulizi zilisema alipelekwa Makongo Sekondari jijini Dar es Salaam. Ghafla ukaibuka mzozo mkubwa baina ya Dogo na Madee, uliosababisha Chalii kurudi zake Arusha. Sina sababu ya kurudia maneno yaliyoibuliwa na pande zote mbili wakati ule kila mmoja akijisafisha mbele ya macho ya watu.
Lakini kifupi Dogo Janja alilia kufanywa mgodi, akitumika kumtengenezea hela Madee, kwamba alipiga shoo nyingi, lakini kipato akawa hakioni, kinaishia kwa mkubwa. Na Madee naye alifunguka, akimlaumu Dogo kwa kuzuzuka na jiji, kuacha shule na tabia nyingine mbaya.
Kwa sababu zilizo wazi, watu wengi walimuunga mkono Dogo Janja, wakamsifu kwa kujitambua. Lakini bahati mbaya, baada ya kutoka Tip Top, akadondokea Mtanashati Entertainments ambako baadaye taarifa zilisema alifukuzwa kwa makosa yanayofanana na yale yaliyowahi kutolewa na Madee.
Habari ambazo bado hazijathibitishwa, zinasema kijana wetu amenyoosha mikono, anataka kurejea tena Tip Top Connection, kule kule ambako ‘Rais wa Manzese’ ndiye mfalme.
Kama nilivyosema pale awali, Dogo Janja bado ni kijana mdogo kwa umri. Sanaa aliyochagua inahitaji mtu aliyetulia kichwani ili aweze kufanikiwa. Kitu ambacho kingeweza kumsaidia kupata mwongozo bora katika maisha yake, ni elimu pekee.
Ni jambo linalosikitisha kusikia kwamba anakimbia shule. Wakati flani nilisikia alifeli sana katika mtihani wake, sababu kubwa ikiwa ni kushindwa kuhudhuria vipindi darasani. Kama angetambua kuwa ujinga alionao, ambao yeye anauona ujanja, ndiyo unaomfanya asiende shule, hakika angetazama maili nyingi zaidi mbele na kujirudi.
Muziki wa Bongo umejaa dhuluma kila upande na watu hawa wabaya wamejenga mtandao wa kulinda masilahi yao. Mtandao huu unawahusisha watayarishaji wa muziki (producers), viongozi wa makundi, watangazaji wa redio, maofisa masoko wa kampuni kubwa na hata wasambazaji wa kazi za wasanii.
Msanii anatakiwa kuwa na kichwa kilichotulia kuweza kuushinda mtandao huu. Ndiyo maana wasanii wakubwa kama AY na Mwana FA, licha ya ustaa wao, walitumia sehemu ya mapato yao kurudi shule kujiweka sawa.
Msanii akikorofishana na mmoja kati ya wanamtandao, anaathirika sana. Kwa sababu harekodiwi nyimbo nzuri, kazi yake haichezwi redioni na wala hapewi nafasi ya kufanya shoo.
Kama angekuwa na elimu ya kujitambua, angegundua kwamba wasanii wote, akiwemo Madee mwenyewe wanaibiwa. Unafikiri hawa wanaoongoza makundi wana mapenzi gani na wasanii wawasaidie kutoka, wao wakale wapi?
Na kusoma siyo lazima uwe na digrii, ni kiasi cha kujitambua tu. Ni ile hali ya kujua kwamba kwa jinsi wingu lilivyo, inabidi utembee na mwavuli kwani mvua inaweza kunyesha wakati wowote.
Dogo Janja bado hajachelewa, anao muda mzuri tu wa kuelimika, tena kwa fedha zake mwenyewe. Ningekuwa mimi katika nafasi yake, nadhani ningefanya maajabu, maana muziki ungenipatia elimu ambayo ingeboresha maisha yangu kwa kiwango cha juu kabisa, umri na uwezo wake ni mtaji ambao wengi wanautamani.
Kama amechagua kutembea katika njia hiyo, ambayo kwa bahati mbaya kaka na dada zake nao wanapita, tusitarajie kuwepo kwa mabadiliko, siyo tu ya muziki, bali hata wasanii wenyewe.
Kila siku tutawashuhudia wakiwasujudia watu ambao walipaswa kuwanyenyekea.
chanzo GPL

KALA JEREMIAH AVURUGWA MOYO WAKE

MSANII kutoka jiji la Mwanza ambaye alipata umaarufu kupitia Shindano la BSS amevunja ukimya na kusema mambo mengi juu ya Msanii wa Filamu ambaye wanatoka wote jiji moja la Mwanza ambaye anajulikana kwa jina la Suzane Michael. Kala alifunguka hayo na kusema kuwa "Nawashangaa sana hawa madada zetu yani wao wanaona kujiachia ndiyo wataishi mjini, huyu dada mimi namfanhamu na sikutegemea kama ataweza kupiga picha za hivi na kuziweka mtandaoni yani kwa hiki kitendo ameuvuruga moyo wangu na kuuchafua kabisaaaa" alisema Kala
Mwanadada Suzane Michael Hata ivyo kala alizidi kuongeza "Unajua kule kwetu Mwanza mtoto wa kike anajiheshimu sana na ndiyo maana wanazidi kupendeza ila wakija Dar tu kila kitu kinakuwa nyuma mbele mbele nyuma." aliongezea,
 
chanzo habari kwanza

MVUA YAWATESA WAKAZI WA DAR ES SALAAM

    Mwavuli unaotumiwa na wafanyabiashara wadogowadogo  ukiwa umechukuliwa na maji na kutumbukia kwenye shimo eneo la stendi ya mabasi Ubungo.
         Maji yakiwa yametuhama kwenye shimo stendi ya mabasi Ubungo.
Mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia jana na leo imesababisha maafa kwenye baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam ambapo katika mizunguko ya  kamera yetu  imenasa  eneo la nje ya stendi ya Mkoa, Ubungo maji yakiwa yamejaa kila  pande huku wafanyabiashara wadogo wanaofanyia kazi eneo hilo, miavuli yao na vitendea kazi vikisombwa na maji huku mashimo yaliyokuwa yamechibwa katika utengenezaji wa barabara yakizidi kuporomoka.
chanzoGPL

Wednesday, 26 March 2014

CHIEF KIUMBE AMNYANGANYA GARI DIAMOND

LILE gari aina ya Toyota Land Cruiser V8 alilokuwa akitanua nalo staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ liko sokoni linapigwa bei.
Diamond akiwa ndani ya Toyota Land Cruiser V8 linalopigwa bei kwa sasa.
Gari hilo linalomilikiwa na pedeshee maarufu Bongo, Mohammed Kiumbe ‘Chief Kiumbe’ limewekwa sokoni baada ya staa huyo kuchemsha kutoa fedha za kulinunua pamoja na kupewa muda wa kufanya hivyo.
Awali, iliripotiwa kuwa gari hilo ni mali ya Diamond ambaye alikuwa akitamba nalo kila pembe ya Jiji la Dar huku akijinasibu kwamba amelishalipa fedha za kutosha kwa ‘Big Boss’, Chief Kiumbe.
Wengi waliamini na kumweka Diamond au Sukari ya Warembo katika matawi ya juu kutokana na kumiliki gari hilo lenye thamani kubwa na lililojaa vikorombwezo vingi ndani yake.
Staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Picha za Diamond akiwa ndani ya gari hilo zilionekana kwenye magazeti huku akikaririwa kwamba analimiliki kihalali gari hilo aina ya Toyota Landcruiser V8 lenye thamani ya shilingi milioni mia moja na laki moja (100,100,000).
Siku chache zilizopita, Chief Kiumbe alimnyang’anya Diamond gari hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa staa huyo alishindwa kutoa ‘mpunga’ wa kulinunua pamoja na kukaa nalo kwa muda mrefu.
Baada ya hapo gari hilo likapotea machoni mwa watu kwa kutojulikana lilipokuwa limefichwa ingawaje ilidaiwa kuwa Chief Kiumbe alikuwa ameliweka stoo.
...Gari hilo likiwa sokoni.
Mapaparazi wa Risasi Mchanganyiko walilitafuta gari hilo kwa udi na uvumba, ndipo walipobaini kwamba  lilikuwa limewekwa sokoni katika yadi moja iliyopo maeneo ya Kijitonyama, Dar likipigwa bei.
Waandishi wetu walifika katika yadi hiyo na kujifanya wanunuzi na kuambiwa kuwa gari hilo lilimshinda Diamond.
“Hili gari lina vitu vingi vizuri, ukiwa na ‘sensa’ ndipo unapoweza kuondoka nalo kwa sababu halitumii funguo, bila hivyo huwezi, Diamond ameshindwa kulinunua,” alisema jamaa aliyekutwa katika yadi hiyo.
Waandishi hao walitajiwa bei na kupewa nafasi ya kulikagua gari hilo kila kona, hatimaye waliondoka ndani ya yadi hiyo wakiahidi kurudi na mkwanja ili kufanya kile kilichomshinda Sukari ya Warembo.
CHANZO GPL

WARIOBA AFUGUKA



 
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta (kulia) akiongoza kikao cha kwanza cha Kamati ya Uongozi ya Bunge hilo, mjini Dodoma jana.  
 
Dar es Salaam. Wakati Ikulu ikitangaza kwamba Rais Jakaya Kikwete amevunja Tume ya Mabadiliko ya Katiba, tume hiyo imetoa ufafanuzi wa baadhi ya maeneo ya Rasimu ya Katiba.
Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana, ilieleza kuwa Tume ya Jaji Joseph Warioba ilivunjwa tangu Machi 19, ikiwa ni siku moja baada ya kuwasilisha Rasimu ya Katiba bungeni mjini Dodoma.
Wakati taarifa ya Tume ya Warioba ilitolewa jana jioni, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilikuwa imeshatoa taarifa ya kuvunja tume hiyo mapema jana ikieleza kuwa shughuli za tume hiyo zilikoma tangu  Jumatano iliyopita.
“Kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Rais wa Jamhuri ya Muungano alivunja rasmi Tume ya Mabadiliko ya Katiba tarehe 19 Machi, 2014 kwa Tangazo la Serikali Na.81 la tarehe 21 Machi, 2014,” ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.
Hata hivyo,  Jaji  Warioba aliliambia gazeti hili jana kuwa hadi wanakutana juzi kwenye kikao cha mwisho cha tathmini walikuwa hawajapokea barua ya kuvunjwa kwa tume yake.
“Barua ya Ikulu tumeipokea leo. Tulikuwa hatuna taarifa kwamba tume yetu imevunjwa hadi tulipopokea barua leo (jana). Tulifanya kikao chetu cha mwisho cha tathmini jana (juzi),”  alisema Warioba alipozungumza na Mwananchi jana jioni.
Warioba pia alithibitisha kwamba taarifa ya ufafanuzi (imechapishwa ukurasa wa 37) ni ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
<MWANANCHI>

DIOMOND AVALISHWA WIGI


Wema baada ya kuhangaika kulitafuta wigi lake, hatimaye akambamba baby wake kalivaa Lol, akampiga picha, akaitupia Instagram
CHANZO GPL

Monday, 24 March 2014

NJEMBA ANASWA NA MKE WA RAFIKI YAKE


Mke wa mtu sumu: Anton John Mwaweje baada ya kunaswa akiwa na mke wa rafiki yake gesti.
Tukio hilo lilijiri mwanzoni mwa wiki hii kwenye gesti moja maarufu (jina tunalo) iliyopo Buguruni- Malapa jijini Dar es Salaam.
Katika sakata hilo ilidaiwa kuwa, Mwaweje alikuwa akiifahamu vyema familia ya Chalz sambamba na mke wake (jina lipo) lakini hilo hakulijali na kumtokia mke wa Chalz ambaye kwa utamaduni wa Kiafrika ni shemejiye.
Mshangao: Anton John akishangaa baada ya kuba
Habari zikazidi kudai kwamba, ilifika mahali katika kumtaka shemejiye huyo ambaye alikuwa akimkatalia katakata, Mwaweje alitumia gia nyingine ikiwemo ya kumuahidi mambo manono kama angekubali kuivunja amri ya 6 ya Muumba na yeye.
Chanzo cha habari kiliendelea kudai kuwa,  ‘Mungu si Athuman wa Lucas’ siku isiyo na jina jamaa alimtumia ujumbe (SMS) mke wa mwenzake kwa kutumia maneno ya kumtoa nyoka pangoni kumbe muda huo bwana simu alikuwa nayo mwenye mke.
Misosi na mitungi: Baadhi ya misosi na vinywaji vilivyokutwa chumbani humo.
Chalz alimwita mkewe na kumuuliza ni nani aliyemtumia ujumbe huo? Ndipo mke akaanika ukweli akisema:
“Mume wangu, wala usikonde. Aliyetuma ujumbe huo si mwingine, ni Anton…”
Mume:  “(akihamaki) Anton huyuhuyu?”
Mke: “Huyuhuyu mume wangu. Amekuwa akinitaka kimapenzi kwa muda mrefu sana, namkatalia lakini hasikii.”
Za mwizi 40: Bwana Anton John akiwa na pingu mkononi baada ya kunaswa na kamanda wa OFM pamoja na wanausalama.
Pia, mwanamke huyo alimwonesha mumewe meseji kibao ambazo jamaa huyo amekuwa akimtumia na zile ambazo yeye amekuwa akimkatalia.
“Sasa sikia, mkubalie,” mwanaume huyo alimwambia mke wake huku midomo ikimcheza kwa hasira.
Chini ya usimamizi wa mumewe, mwanamke huyo aliwasiliana na Anton na kumwambia alikuwa na nafasi wanaweza kukutana kwa ajili ya kumsaliti Chalz.
Baada ya kupanga mipango ya kukutana, mume huyo alipiga simu Global Publishers kwenye kitengo cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) na kuomba msaada wa fumanizi ambapo alibahatika kukuta kuna kamera mpya zimewasi tayari kwa kazi kama hizo.
Baada ya kupata maelezo ya Chalz, OFM ilishirikiana na Jeshi la Polisi Buguruni –Kwamnyamani jijini Dar na kuandaa mtego ambapo Jumatatu iliyopita, saa nane na ushee mchana, Anton ambaye naye inasemekana ana mke aliuingia mtego na kunasa kwenye chumba namba 5 akiwa na mke mwema huyo.
Ndani ya chumba hicho, Anton alikutwa na boksa  tayari kwa mlo wa wizi ambao alibakia kuendelea kusikia njaa. Mezani, kulikuwa na chipsi kuku na pombe ambazo zingewapa stimu kabla ya mchezo.
Kitendo cha Chalz kumnasa jamaa huyo na mkewe kitandani kilimpandisha munkari ambapo nusura afanye ndivyo sivyo lakini alitulizwa na polisi waliokuwa eneo hilo kwa ajili kulinda usalama.
Kilichofuata baada ya hapo, mgoni huyo akiwa na pingu mkononi alipelekwa kwenye kituo hicho cha polisi ambapo awali, Chalz alitoa ripoti ya malalamiko baada ya kugundua  jamaa huyo anataka kumtumbukiza mkewe kwenye mstari wa usaliti.
Mpaka OFM wanaondoka kituoni hapo, taratibu za kisheria kuhusiana na kesi hiyo zilikuwa zikiendelea huku mgoni huyo akiwa chini ya ulinzi mkali.
CHANZOGPL

NDEGE MALAYSIA IMEPOTELEA KUSINI MWA BAHARI YA HINDI

Waziri Mkuu wa Malaysia Najib Razak akitangaza leo juu ya utafiti wa rada kuonyesha kuwa ndege iliyopotea imeangukia katika bahari ya Hindi.
Tangazo hilo limetolewa wakati ndege ya majini ya Australia ikiwa njiani kuelekea kunakoonekana vitu hivyo vilivyoonwa na ndege za kijeshi wakati wa msako wake.
Wanajeshi wa jeshi la Australia wakiwa ndani ya ndege katika kituo cha Kijeshi cha AP-3C Orion.
WAZIRI Mkuu wa Malaysia, Najib Razak ametangaza habari mpya kwamba ndege ya abiria iliyopotea ilimalizia safari yake kusini mwa bahari ya Hindi, tangazo ambalo limewavunja moyo wanandugu wa abiria.
Ndege hiyo ya abiria ya Malaysia iliyokuwa na namba MH370 ilitoweka katika rada za kiraia saa moja baada ya kuruka kutoka Kuala Lumpur kuelekea  Beijing ikiwa na watu 239 ndani yake hapo Machi 8 mwaka huu.
Hakuna habari zilizothibitishwa juu ya kuonekana kwa mabaki ya ndege hiyo, ingawa kumekuwa na vitu vinavyoonekana huko pwani ya Australia vinavyodhaniwa huenda ni sehemu ya chombo hicho. Ndugu wa abiria waliokuwemo ndani, wameanza mipango ya kusafiri kuelekea huko.
Hata hivyo, vitu vilivyoonekana kwenye satellite ya China na Ufaransa, bado havijaweza kufikiwa na kutambuliwa kama vina uhusiano wowote na ndege hiyo ambayo ni gumzo kwa sasa duniani.
CHANZO NI DAILYMAILY

WATU 529 WAHUKUMIWA KIFO



Wafuasi wa Muslim Brotherhood.
Mahakama nchini Misri imewahukumu kifo watu 529 ambao wanasemekana kuwa wafuasi wa Rais aliyeng'olewa mamlakani Mohammed Morsi.Watu hao walikabiliwa ma mashitika mbali mbali yakiwemo mauaji ya polisi na kuwavamia polisi.
Wafuasi hao wa chama kilichopigwa marufuku, cha Muslim Brotherhood, ni sehemu ya kundi lengine kubwa la watu zaidi ya 1,200 wanaoaminika kuwa wafuasi wa Morsi.Maafisa wa utawala nchini Misri wamekuwa wakiendesha msako mkubwa dhidi ya wafuasi wa vuguvugu hilo, tangu Morsi kuondolewa mamlakani mwezi Julai mwaka jana.
Maelfu wamekamatwa huku mamia wakiuawa.Mahakama hiyo ilitoa hukumu baada ya vikao viwili pekee ambapo mawakili wa watuhumiwa walilalamika kuwa hawakupewa muda wa kuwasilisha kesi yao vyema.
Mauaji wanayodaiwa kufanywa na watuhumiwa yalitokea Kusini mwa Misri, mwezi Agosti, baada ya vikosi vya usalama kuvunja kambi mbili za wafuasi wa Morsi waliokuwa wanataka arejeshwe mamlakani.
CHANZO: BBC SWAHILI

WAAMUZI WATAO AFRIKA KUCHEZESHA KOMBE LA DUNIA

Afrika itawakilishwa na waamuzi wa kati watatu kwenye fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Brazil kwa mujibu wa orodha ya waamuzi 25 iliyotolewa na Shirikisho la Soka Kimataifa (FIFA. Kila mwamuzi ataongoza timu ya wasaidizi wawili na hivyo kufanya idadi ya waamuzi wasaidizi kutoka Afrika kuwa nane kati ya 50.
Fainali za Kombe la Dunia 2014 zitafanyika nchini Brazil kuanzia Juni 12 mpaka Julai 13 ikiwa ni mara ya pili kwa fainali hizo kufanyika kwenye nchi hiyo kigogo katika soka duniani. Mara ya kwanza fainali hizo zilifanyika Brazil mwaka 1950.
Waamuzi hao ni Doue Noumandiez kutoka Ivory Coast, Papa Gassama (Gambia) na Djamel Haimoudi (Algeria) ambao wataongoza timu ya waamuzi watatu kila mmoja kwenye fainali hizo, kwa mujibu wa utaratibu wa FIFA.
Doue atachezesha mechi za fainali hizo pamoja na waamuzi wasaidizi kutoka Burundi, Songuifolo Yeo na Jean Claude Birumushahu.
Gassama ataunda timu itakayowajumuisha waamuzi wasaidizi Evarist Menkouande kutoka Cameroon na Kabanda Felicien kutoka Rwanda, wakati Haimoudi ataongoza waamuzi wasaidizi Abdelhak Etchiali wa Algeria na Redouane Achik wa Morocco.
Mwamuzi wa akiba kutoka Afrika Kusini Daniel Bennett na Neant Alioum kutoka Cameroon wanakamilisha orodha hiyo ya waamuzi kutoka Afrika. Katika orodha hiyo pia wamo Djibril Camara (Senegal) na Marwa Range (Kenya).
Afrika imeendelea kushikilia idadi yake ya waamuzi watatu wa kati kwenye fainali hizo.
Kwa mujibu wa orodha ya FIFA waamuzi wengine ni Ravshan Irmatov kutoka Uzbekistan, Yuichi Nishimura (Japan), Nawaf Shukralla (Bahrain), Benjamin Williams (Australia), Joel Aguilar (El Salvador), Mark Geiger (Marekani), Marco Antonio Rodriguez (Mexico), Enrique Osses (Chile), Nestor Pitana (Argentina), Sandro Ricci (Brazil), Wilmar Roldan (Colombia), Carlos Vera (Ecuador), Peter O’Leary (New Zealand), Felix Brych (Ujerumani), Cuneyt Cakir (Uturuki), Jonas Eriksson (Sweden), Bjorn Kuipers (Uholanzi), Milorad Mazic (Serbia), Pedro Proenca (Ureno), Nicola Rizzoli (Italia), Carlos Velasco (Hispania) na Howard Webb (England).
Mbali na Afrika, bara la Ulaya litatoa waamuzi tisa, Shirikisho la Soka la Amerika ya Kusini (CONMEBOL) litatoa waamuzi watano, huku waamuzi wanne wakitoka Asia (AFC), watatu kutoka Shirikisho la Soka la vyama vya Amerika ya Kaskazini na Visiwa vya Carribea (CONCACAF) na mmoja kutoka Oceania.
Akizungumzia uteuzi wa waamuzi hao 25, Katibu Mkuu wa Fifa, Jerome Valcke alisema: “Waamuzi hao walichaguliwa kutokana na uwezo wao, uelewa wao wa mchezo wa soka, uwezo wa kuusoma mchezo na kuelewa timu zinazocheza zinatumia mbinu gani.”
Hata hivyo Valcke alisema kuna baadhi ya waamuzi na wasaidizi wao wanaweza kuachwa Juni 12 wakati watakapowapima kwa mara ya mwisho ili kujua kama wapo fiti kabla ya kuanza kwa mashindano.
Alisema: “Fifa ina utaratibu wa kuchagua waamuzi bora ambao wapo fiti kwa ajili ya kuchezesha Fainali za Kombe la Dunia. Huwa tunachagua waamuzi ambao wapo katika ubora wa juu kabla ya mashindano.”

< mwananchi>

WAJUMBE BUNGE LA KATIBA NJIAPANDA

 
“Kama tunataka serikali ya tatu lazima tuitengenezee misingi ya uhakika na kuhoji nani atayeidhamini serikali ya tatu virungu, pingu, magari ya kuwasha, majeshi au bunduki.”PICHA|MAKTABA. 

Dar es Salaam. Kwa neno moja unaweza kusema kwamba wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na wananchi kwa ujumla wako “njiapanda”.
Hii ni baada ya hotuba ya ufunguzi wa Bunge hilo iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete kuibua mambo mazito ambayo kimsingi yanatofautiana na mapendekezo yaliyomo katika Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Huku wananchi wakijiuliza nini hatima ya Bunge hilo baada ya hotuba hiyo, baadhi ya wajumbe ambao wiki hii ndiyo wanaanza kujadili rasimu hiyo, watakuwa katika wakati mgumu wa kuamua wafuate maoni ya nani, kati ya viongozi hao wawili.
Ingawa Rais Kikwete amesema mara kadhaa kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba ndiyo waamuzi. Mambo mengi aliyoibua yanaonyesha kutokubaliana kwake na baadhi ya maoni ya wananchi yaliyomo katika rasimu, ambayo Jaji Warioba amewahi kusema kuwa yanatakiwa kuheshimiwa.
Wakizungumzia tofauti hizo, mjumbe wa Bunge la Katiba, Ezekiah Oluoch alisema kauli za Rais Kikwete na Jaji Warioba zimezidi kuwagawa wajumbe wa Bunge hilo kwa maelezo kuwa tangu awali wajumbe hao walikuwa wamegawanyika katika makundi mawili; ya wanaotaka muundo wa Muungano uwe wa serikali tatu na wale wanaotaka serikali mbili.
Alisema kama suala la muundo wa Serikali likishindikana kupatiwa mwafaka ni vyema likarudishwa kwa wananchi ili wapige kura ya maoni kuchagua aina wanayoitaka, kisha suala hilo lirejeshwe tena katika Bunge la Katiba kwa ajili ya kuboreshwa.
“Rais alipoanza kuzungumza alikuwa kama mkuu wa nchi lakini mwisho wa hotuba yake aligeuka kuwa mwenyekiti wa CCM. Kifupi alichokizungumza kimekwenda tofauti na wadhifa wake,” alisema.
Naye Deo Filikunjombe alisema: “Nadhani kwa hotuba hizi mbili, kazi ya wajumbe wa Bunge la Katiba itakuwa rahisi. Maana sasa wameshajua uzuri na ubaya wa serikali tatu na mbili.
“Hata kama kutakuwa na tofauti, wananchi ndiyo watakuwa wa mwisho kuamua kama Katiba hii ipite au isipite. Tunachotakiwa wajumbe ni kuwa makini na uamuzi wetu.”
Naye Yusuf Manyanga alisema: “Bunge la Katiba limejaa watu wenye busara. Sidhani kama tutashindwa kuelewana maana hata katika biashara ya utumbo inzi ni wengi lakini utumbo unauzika.”
Katika hotuba yake aliyoitoa Ijumaa iliyopita Rais Kikwete aligusia mambo saba ya msingi yaliyomo katika rasimu ya Katiba na kutaka yatazamwe kwa kina, huku akibainisha kuwa mengine hayawezekani kutekelezeka.
<mwananhi>

Sunday, 23 March 2014

WARIOBA AMFURAHISHA MTIKILA

 Mchungaji Christopher Mtikila.PICHA|MAKTABA 

Dodoma. Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mchungaji Christopher Mtikila amesema madai yake ya zaidi ya miaka 20 kuhusu Serikali ya Tanganyika yamerahisishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na ana imani Tanganyika inarejea muda mfupi ujao.
Akizungumza na gazeti hili nje ya viwanja vya Bunge, Mchungaji Mtikila, alisema amefarijika kuona Jaji Warioba amewafahamisha Watanzania kuhusu ukweli wa Muungano, hivyo wanaweza kuelewa sasa sababu za yeye kudai Tanganyika.
 “Naamini sasa Tanganyika inarudi, lakini watu wachache wakizuia safari hii nitakwenda Mahakama ya Umoja wa Mataifa kudai Tanganyika kwani ndio ilipigania uhuru na tayari nina mawakili,” alisema.
Aliongeza  kuwa Jaji Warioba ameunga mkono hoja  ya kudai Tanganyika kwani haiwezi kupotezwa na watu wachache kwani tayari Zanzibar imejitangaza kuwa ni nchi  huru ndani ya Muungano.
Alisema Muungano ni suala la hiari, hivyo viongozi wachache wa chama tawala hawawezi kulazimisha Muundo  wa Muungano ambao unapingwa na mamilioni ya Watanzania.
“Naamini wale waliokuwa wamechomwa sindano za usingizi wa miaka yote sasa watafufuka na kuungana na wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika na sasa imekuwa koloni la Zanzibar,” alisema Mtikila.
Alisema muundo wa Muungano uliopo sasa wa serikali mbili ni kongwa la utumwa wa kikundi cha watu wachache ndani ya CCM ambao ndio wananufaika.

mwananchi