SIMBA imefanya usajili mwingine wa kimyakimya baada ya kumsajili mshambuliaji raia wa Gambia.
Mshambuliaji huyo ametajwa kwa jina la Omar Mboob aliyewasili jana usiku kwa Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.
Ingawa viongozi wa Simba hawakuwa wakipokea simu jana, taarifa za
uhakika zinaeleza mshambuliaji huyo kinda anatarajia kuanza mazoezi leo
na Simba.
“Kweli Simba wamekuja usiku wa jana (juzi) wakampokea mchezaji mmoja na wamesema anatokea Gambia.
“Walikuja na Hiace yao hapa wakampokea na kuondoka naye lakini
walifanya mambo yao harakaharaka utafikiri kuna jambo la
uficho.“Nilimsikia kiongozi mmoja akitaka waondoke haraka hapa airport
kwa kuwa waliwahofia Yanga,” kilieleza chanzo cha uhakika kutoka Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa Kamati ya Utendaji ya Simba alipoulizwa jana,
alionekana kushangazwa na swali hilo, lakini hakutoa jibu.“Nani
kakuambia, mimi sijui lolote. Wamekuambia anatokea nchi gani? Ila ukweli
sina habari ndugu yangu,” alisema.
Ila taarifa za uhakika, zinasisitiza mshambuliaji huyo amefichwa na
viongozi wa Simba wamekuwa wakifanya siri kubwa kuhakikisha haijulikani.
Lengo ni kuepuka Yanga au klabu nyingine kuingilia kati ili wajaribu
kuona kiwango cha mchezaji huyo kutokea katika Jiji la Banjul,
Gambia.Iwapo Mgambia huyo atafuzu, basi itakuwa ni hatari kwa Warundi,
Amissi Tambwe na Pierre Kwizera kwa kuwa mmoja wao atalazimika kuachia
nafasi.SI
Saturday, 6 December 2014
CHRISTIAN KUFUNIKA DAR
Stori: ShowbizWAKATI siku zikizidi kukatika kuelekea Desemba 6, katika ule Usiku wa Nani Kama Mama ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem, jijini Dar ambapo Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’ anatarajiwa kuweka historia mpya ndani ya ukumbi huo.

Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’.
Akipiga stori na Showbiz, Meneja wa Bella, Amiri Marusu
aliongelea usiku huo ambao umekuwa gumzo kubwa kwakuwa ni mara ya kwanza
kufanyika uzinduzi wa Albamu ya Nani Kama Mama ndani ya Dar Live hivyo
Bella amejipanga vya kutosha kwa kuweka historia mpya ukumbini hapo.
“Mashabiki wakae mkao wa kusikia ngoma kali zote kama vile Hanitaki
Tena, Usilie aliyoimba na Banana Zoro, Msaliti, Nakuhitaji na nyingine
kibao ambazo zipo katika albamu hiyo,” alisema Amiri.
Christian Bella ‘Obama’ akipozi.
Bella ambaye alitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kutua
katika bendi ya Akudo Impact na kutengeneza ngoma kali kama Walimwengu
si Wanadamu, Bomoa Bomoa, Safari Sio Kifo, Yako Wapi Mapenzi na nyingine
nyingi. Ametokea kujizolea umaarufu kwa sauti nyingi tofauti kiasi cha
kupelekea kutungiwa jina la Mfalme wa Masauti.Saturday, 11 October 2014
JEMBE KINANA AENDELEA KUVUNJA CHADEMA
Katibu Mkuu wa CCM,
Abdulrahman Kinana akionesha kadi 27 za wananchama wa Chadema
waliokihama chama hicho na kujiunga na CCM kaatika mkutano wa hadhara
uliofanyika Mjini Nyololo, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama
na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010. Kulia aliyevaa
shati jeupe ni aliyekuwa Katibu wa Kata ya Igowole, Josephat Soda ambapo
wengine ni miongoni mwa walio kuwa wafuasi wa Chadema.
Aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Igowole, Joephat Soda akikabidhi bendera ya chama hicho kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya yeye na wenzie 26 kutangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo.
Kinana akimkabidhi kadi ya CCM, Josephat Soda baada ya kutanga kujiunga na CCM katika mkutano huo.
Josephat Soda akielezea jinsi alivyoamua kuondoka Chadema na kujiunga na CCM, ambapo alisema amechoka na chama kilichosheheni uongo, ambapo viongozi wa Chadema alidai kuwa walitoa maagizo kuwaakope fedha za kujengea Mnara wa mwandishi wa habari Marehemu David Mwangosi, aliyeuawa wakati wa vurugu za Chadema na Polisi katika Mji wa Nyololo, ambapo walimuahidi kumtumia fedha zilizotumika kujenga mnara huo ahadi ambayo hadi sasa haalipwa na anadaiwa na muuza simenti na muuza saruji alikokopa. CCM imeamua kulipa madeni yote aliyokuwa akidaiwa.
Wanachama wa CCM wakiwemo wapya kutoka Chadema, wakiapa kiapo cha utii cha CCM baada ya kukabidhiwa kadi wakati wa mkutano huo.
Aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Igowole, Joephat Soda akikabidhi bendera ya chama hicho kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya yeye na wenzie 26 kutangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo.
Kinana akimkabidhi kadi ya CCM, Josephat Soda baada ya kutanga kujiunga na CCM katika mkutano huo.
Josephat Soda akielezea jinsi alivyoamua kuondoka Chadema na kujiunga na CCM, ambapo alisema amechoka na chama kilichosheheni uongo, ambapo viongozi wa Chadema alidai kuwa walitoa maagizo kuwaakope fedha za kujengea Mnara wa mwandishi wa habari Marehemu David Mwangosi, aliyeuawa wakati wa vurugu za Chadema na Polisi katika Mji wa Nyololo, ambapo walimuahidi kumtumia fedha zilizotumika kujenga mnara huo ahadi ambayo hadi sasa haalipwa na anadaiwa na muuza simenti na muuza saruji alikokopa. CCM imeamua kulipa madeni yote aliyokuwa akidaiwa.
Wanachama wa CCM wakiwemo wapya kutoka Chadema, wakiapa kiapo cha utii cha CCM baada ya kukabidhiwa kadi wakati wa mkutano huo.
<<<<<<<<GPL>>>>>>>>
JAMBAZI SUGU LAUWAWA ARUSHA
Wakazi wa Jiji la Arusha wakiwa katika Kituo cha Polisi mkoani humo
kushuhudia mwili wa mtu anayedaiwa kuwa jambazi sugu, Ramadhan Abdallah
Jumanne (Rama Ndonga), aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi usiku wa
kuamkia jana. Picha na Happy Lazaro.
Mtu huyo aliyefahamika kwa kwa jina la Ramadhan
Abdallah Jumanne maarufu kama Rama Ndonga (37) Mkazi wa Moivo hatimaye
ameuawa polisi baada ya kupigwa risasi katika majibizano na askari wa
jeshi hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema jambazi
huyo aliuawa usiku wa kuamkia jana majira ya saa 2:04 usiku katika
Kijiji cha Moivo, Kitongoji cha Enaboishu wilayani Arumeru.
Alisema baadhi ya matukio ya ujambazi aliyowahi
kuhusika nayo ni lililotokea Agosti 6 mwaka huu saa 3:30 usiku maeneo ya
Kwa Iddi ambapo walimpiga risasi sehemu ya shingo mwanamke Shamimu
Rashid aliyekuwa Mkazi wa Sakini wakati akijiandaa kuingia nyumbani
kwake na kumuua.
Kamanda Sabas alitaja tukio lingine ni la Agosti
21 mwaka huu majira ya saa 1:00 huko maeneo ya Olasiti, jambazi huyo
akiwa na mwenzake kwenye pikipiki walimjeruhi kwa kumpiga risasi ya
mdomoni na kutokea kichwani mtoto Christen Nickson mwenye umri wa miaka
mitatu na nusu na kisha kufanikiwa kupora Sh200,000 na baadaye majeruhi
huyo alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount
Meru.
Aidha, kukamatwa kwa jambazi huyo ni baada ya
polisi kutumia mbinu za kisasa na kufika nyumbani kwa marehemu na polisi
walimwamuru ajisalimishe lakini alikaidi na kuanza kuwarushia risasi
hali iliyosababisha askari kujibu mapigo na hatimaye kusababisha kifo
chake.
Alisema kuwa, baada ya upekuzi mwili wa marehemu
ulipatikana na bastola aina ya Glock 19 yenye namba RLU 976
iliyotengenezwa nchini Australia ikiwa na magazine yenye risasi 14
ambayo alikuwa ameishika mkononi pamoja na maganda matano ya risasi.
Aidha, upekuzi zaidi uliofanywa katika chumba
chake ulibaini magazine moja yenye risasi 15 na magazine mbili zenye
uwezo wa kubeba risasi 30 kila moja, redio call moja yenye nembo ya
ITSS/UNICTR, pikipiki aina ya Toyo Power King rangi nyekundu yenye namba
za usajili T 507 BSU.
Upekuzi zaidi ulibaini kofia ngumu ya kuendesha
pikipiki rangi nyekundu, plate number ya pikipiki yenye namba T 805 CVD,
pingu moja, Glock Fab Defence moja na vifaa vya kusafishia bastola
pamoja na koti jeusi.
Kamanda Sabas alisema polisi wanaendelea kumsaka
mwenzake waliyekuwa wakitumia naye pikipiki hiyo, ili kuweza kuutokomeza
mtandao huo ambao umekuwa tishio jijini Arusha.
Kutokana na tukio hilo, watu walifurika kituo cha polisi kushuhudia mwili wa marehemu ambaye aliutikisa mji huo.
POLICE 120 WATIMULIWA CHUONI MOSHI

Moshi. Maofisa wa Polisi wapatao 120 wa Jeshi la Polisi, waliokuwa wakihudhuria mafunzo ya kupandishwa vyeo katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA), wametimuliwa chuoni hapo.
Habari za uhakika zilizopatikana jana kutoka ndani
ya chuo hicho zamani kikijulikana kama CCP, zimedai uamuzi wa kuwaondoa
chuoni ulitangazwa jana na mkuu wa chuo hicho, Matanga Mbushi.
Vyanzo mbalimbali vililidokeza gazeti hili kuwa,
waliotimuliwa chuoni hapo ni maofisa ambao wana ulemavu wa aina
mbalimbali walioupata wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi.
Habari hizo zilisema hadi jana saa 9:00 alasiri,
maofisa hao walikuwa ofisi za mkuu wa chuo hicho wakisubiri kupatiwa
maelekezo ya namna ya kurejea katika vituo vyao vya kazi mikoa
mbalimbali.
“Wako 120 hivi walikuja hapa (MPA) kwa ajili ya
kuchukua kozi za Koplo, Sajenti, Meja na ‘Assistant Inspector’ (wakaguzi
wasaidizi), lakini ndiyo hivyo wametuambia tuondoke,” kilidokeza chanzo
chetu.
Hata hivyo, ofisa mmoja alilidokeza gazeti hili
kwamba mkuu wa zamani Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, ambaye
amestaafu, ndiye wa kulaumiwa kwa kutoheshimu mapendekezo ya wataalamu.
“Tulimwambia IGP Mwema kwamba ni vizuri kama
maofisa wenye ulemavu kama baadhi ya vigezo wanavyo basi wapewe vyeo
huko huko mikoani, lakini wasiende chuoni,” alidokeza na kuongeza;
“Tulipendekeza yafunguliwe madarasa ya kanda
wakishafanya mtihani wa kawaida wapewe vyeo huko huko, lakini wakija
chuoni ni lazima wahudhurie vipindi vyote ambavyo vinafanya chuo kiitwe
chuo.
“Chuo chochote kile kina vigezo vyake na kwamba
ili mtu apate cheo alichokwenda kukisomea ni lazima ahudhurie asimilia
95 ya vipindi ikiwamo kwata, medani za kivita na kuzuia vurugu,”alisema.
Chanzo kingine kililidokeza gazeti hili kuwa
maofisa hao waliripoti chuoni hapo wiki mbili zilizopita na katika
uchunguzi, walibainika wana ulemavu ambao hawawezi kumudu mafunzo ya
ukakamavu.
Mmoja wa maofisa hao waliotimuliwa alilalamika
kuwa kitendo hicho siyo cha kiungwana kwa kuwa ulemavu huo waliupata
wakiwa kazini wakilitumikia Taifa na hawajashindwa kuingia darasani.
“Baadhi yetu tumefanya kazi miaka 20 wengine 25.
Wamekatika miguu. Wako trafiki wamegongwa na polisi wengine wamepigwa
risasi na majambazi wakapata ulemavu si sawa kutunyima vyeo,”
Monday, 22 September 2014
SIMBA KAKABWA KOO NA WAGOSI WA KAYA
inShare
Dar es Salaam. Makosa ya mabeki
wa Simba yaliyofanywa dakika za majeruhi, yaliipa sare ya kwanza msimu
huu baada ya kufungana 2-2 na Coastal Union ya Tanga katika mechi ya
kupendeza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.Katika mchezo huo, Coastal walitumia dakika nane
za majeruhi kipindi cha pili kufunga bao la kusawazisha na kuinyima
Simba ushindi katika mechi yao ya kwanza msimu huu.Bao la Coastal lilitokana na makosa ya kiufundi ya
mabeki wa Simba walioshindwa kuweka ukuta imara kuzuia kiki ya adhabu
ndogo iliyopigwa na Ramadhan Salum dakika ya 82 na kwenda moja kwa moja
kwenye kamba za Wekundu hao.
Kosa la kwanza lililoigharimu Simba na kuipa
Coastal kupata bao la kwanza, lilifanywa na kiungo Pierre Kwizera
aliyeshindwa kuumiliki vizuri mpira kabla ya kunaswa na wachezaji wa
Coastal Union na Lutimba Yayo Kato kuutumbukiza wavuni kwa kiki ya
karibu na lango.
Kwa matokeo ya mchezo wa jana, Simba na Coastal Union zimezoa pointi moja kila mmoja.
Mchezo wa jana uliokamilisha mechi za kwanza za
raundi ya kwanza ya ligi hiyo, ulianza kwa Simba kusalimia lango la
wapinzani wao na kuandika bao la kwanza kupitia kwa Shaaban Kisiga.
Kisiga alifunga bao hilo kwa mpira wa faulo dakika ya saba kabla ya Amis
Tambwe kufumania nyavu dakika ya 36 akiunganisha kwa kichwa akimalizia
krosi ya Emmanuel Okwi.
Kwa upande mwingine, juhudi za Simba kupata mabao,
zilichangiwa kwa kiasi kikubwa na Okwi kwani bao la kwanza, aliangushwa
nje ya 18 na beki wa Coastal, Tumba Swedi kabla ya Kisiga kufunga kwa
faulo, pia alipiga krosi ambayo iliunganishwa na Tambwe kuandikia bao la
pili.Jitihada za Union kusaka bao zilizaa matunda katika dakika ya 67
baada ya Lutimba Yayo Kato kufanikiwa kumtungua kipa wa Simba, Ivo
Mapunda kufuatia pande la Itubu.
Ikishambulia mfululizo, Coastal Union ilisawazisha
dakika ya 82 kupitia kwa Ramadhan Salum aliyetandika mpira wa faulo
uliokwenda moja kwa moja nyavuni.
Simba waliianza mechi ya jana kwa kasi huku
wakitawala sehemu ya kiungo, lakini mipira yao ya mwisho haikuwa makini
na hivyo kushindwa kutengeneza nafasi za mabao huku Haruna Chanongo
akipoteza chache walizozipata.
Katika kipindi cha kwanza, Coastal walitumia muda
mwingi kulinda lango zaidi kuliko kushambulia, huku pia ikifanya
mashabulizi ya kushtukiza wakimtumia mshambuliaji Itubu Imbem.
Kipindi cha pili, Simba walifanya mabadiliko kwa
kuwatoa Chanongo na Tambwe na nafasi zao kuchukuliwa na Uhuru Selemani
na Rafael Kiongera, wakati Coastal waliwatoa Seleman Kibuta, Razak
Khalfan na Joseph Mahindi na nafasi zao kuchukuliwa na Lutimba Yayo
Kato, Ayoub Yahaya na Abbas Athuman.
Mabadiliko hayo yaliwanufaisha Coastal kwani
walipata mabao mawili. Akizungumza baada ya mechi kumalizika kocha wa
Simba, Patrick Phiri alisema: “Coastal walicheza vizuri, sijafurahia
matokeo tuliyoyapata ila tutajiandaa kwa ajili ya mechi ijayo.”
MAN U YABAMIZWA 5
V
London, England. Leicester City ilitoka nyuma
kwa mabao 3-1 na kuibuka na ushindi wa mabao 5-3 dhidi ya Manchester
United katika mchezo wa Ligi Kuu England uliochezwa jana.
United walionekana kama wangeibuka na ushindi
wakati Robin van Persie alipofunga bao la mapema kabla ya Angel Di Maria
kufunga la pili, lakini bao la kichwa la Leonardo Ulloa lilifanya
matokeo kuwa 2-1 kabla ya Ander Herrera kufunga la tatu kwa United.
Leicester walirudi uwanjani kwa kasi na kupata
penalti iliyofungwa na David Nugent na Esteban Cambiasso alisawazisha
bao la tatu, wakati Jamie Vardy akifunga la nne kabla ya Ulloa kufunga
la tano.
Ikiwatumia washambuliaji watatu, Radamel Falcao,
Wayne Rooney na Robin van Persie, United ilishindwa kucheza vizuri
katika kipindi cha pili na kuiruhusu Leicister kumiliki mpira
walivyotaka.
Bao la Andre Schurrle la kipindi cha pili
lilisawazishwa na Frank Lampard na kufanya mchezo kati ya Manchester
City na Chelsea kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Vijana wa kocha Jose Mourinho walilazimisha sare
hiyo ugenini katika Uwanja wa Etihad na kufikisha pointi 13 kileleni
ikiwa na michezo mitano iliyocheza.
Katika mchezo huo, beki wa pembeni wa City, Pablo
Zabaleta alitolewa kwa kadi ya pili ya njano kutokana na kumchezea
vibaya Diego Costa kipindi cha pili.
Mchezo huo ulionyesha kuwa ungekuwa na kadi
nyekundu baada ya wachezaji saba kuonyeshwa kadi za njano katika kipindi
cha kwanza. Kwa matokeo hayo, Chelsea imeendelea kubaki kileleni mwa
msimamo ikiwa na tofauti ya pointi tatu, ikifuatiwa na Southamptom wenye
pointi 10.
Monday, 8 September 2014
MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA JIMBONI KWAKE
Mh:Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr.Kone wakati wakukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Maabara za Kisasa Katika Shule za Jimbo la Iramba,Hapa ni Shule ya Kijiji cha Usule.Kufikia Tar.31/09/2014 Mkuu wa Mkoa anategemea Kumkabidhi Mh:Rais Jakaya Kikwete Maabara zote za Shule za Sekondari zikiwa zimekamilika ndani ya Mkoa wa SIngida kuendana na Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.
Mh:Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa Kijiji cha Usule waliofika kusikiliza mambo mbalimbali ya Utekelezaji wa Shughuli za Maendeleo.
Kwaya ya akina mama Kiji cha Usule wakitumbuiza mbele ya Mgeni Rasmi Mh:Mwigulu Nchemba(hayupo pichani).
Vijana wakifurahia Ushindi wao katika Michuoano ya MWIGULU CUP,Hii ni timu ya Kijiji cha Usule.
Akina mama wakionesha kadi zao za Chama cha Mapinduzi kuonesha kuwa wao bila CCM haiwezekani.
Wananchi wakishangilia baada ya Kuona Nguzo za Umme zikipita kijijini kwao Ishara kuwa Umeme umewafikia.
Mh:Mwigulu akimsikiliza Mmoja wa Wazee wa kijiji cha Usule.
Mkutano unaendelea huku Mh:Mwigulu nchemba akiwafafanulia mambo mbalimbali ya maendeleo wanakijiji wa Usule,Kubwa ni Usambazaji wa maji hapo Kijijini ambao tayari umekwisha anza,Pia amesisitiza Kusuka nyaya za Umeme wakati huu Umeme unapowekwa kwenye nguzo,Ukiingiza Umeme wakati huu mafundi wakiwa wanasambaza nyaya ni Bei nafuu 27000/= tu.
Ilikukamilisha Ujenzi wa Maabara ya Shule ya Usule Mh:Mwigulu amechangia Mifuko 100 ya Sementi na ameagiza kwenye Upungufu wowote Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi atoe taarifa.Hivyo hivyo amesaidia Uchimbaji wa Bwawa la maji kama Mpango wa Muda mfupi wakati Bomba za Maji zikiendelea Kusambazwa kijiji chote cha Usule.
Baadhi ya Vijaja Kijiji cha Kibaya wakiwa kwenye Jezi zao za MWIGULU CUP.
Mh:Mwigulu Nchemba akikabidhi Mchango wake wa bati 70 kwa Diwani wa kata ya Mbelekesye kwaajili ya kuezeka Madarasa ya shule ya Mbelekesye yaliyoongezwa.Pia amechangia Mifuko 100 na Mbao kwaajili ya kupau madarasa hayo.
Wakati hili likifanyika katika kijiji cha Kibaya,Mh:Mwigulu Nchemba jana alikabidhi Mabati 320 kijiji cha Misuna kwaajili ya Ujenzi wa Zahanati.
Wananchi wakibaya wakifurahia na Mbunge wao.
Wananchi wakibaya wakifurahia na Mbunge wao.OKWI HURU KUCHEZA SIMBA

Wajumbe wa Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya TFF wakiwa katika mkutano jijini Dar es Salaam jana. Picha na Said Khamis.
Dar es Salaam. Utata wa Emmanuel Okwi umemalizwa rasmi na mchezaji huyo wa Uganda sasa yupo huru.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilikutana jana na kupitia masuala mbalimbali ikiwamo mgogoro wa kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi.
Mkataba huo ulipitiwa na kamati ikiwamo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na upande wa Yanga na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa mkataba wa pande mbili haupo kwa sababu Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili.
“Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27 mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote,” alisema Wambura.
Alifafanua kuwa mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), ambapo Kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo, hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja.
Pamoja na Yanga kuwasilisha pingamizi la kuwepo mmoja wa wajumbe katika kikao kwa sababu za kimaslahi (conflict of interests), walifahamishwa kuwa kilichopo mbele ya kamati ni mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, na si usajili.
Pia lilijitokeza suala la Okwi kutakiwa na klabu ya Wadi Degla ya Misri.
Kamati imeiagiza Sekretarieti ya TFF kulifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa katika kikao kijacho.
Hata hivyo mjumbe ambaye Yanga ilimpinga hakushiriki katika kuchangia hoja na kutoa maamuzi.
Uamuzi wa kamati ulifanyika baada ya majadiliano, hivyo hakukuwa na suala la kupiga kura.
Kuhusu pingamizi la Coastal Union kwa Abdi Banda, Kamati imebaini kuwa klabu hiyo imevunja mkataba kati ya pande hizo mbili kwa kushindwa kumlipa mchezaji huyo mshahara wa miezi mitatu mfululizo kama takwa la mkataba.
ZITO :ATOA YA MOYONI
Dar es Salaam. Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameeleza tofauti yake na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akisema imesababishwa na watu aliowaita wapambe.
Zitto (37), ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Chadema, alisema kuwa hata kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya chama kulisababishwa na wapambe hao, lakini akasisitiza kuwa hana kinyongo tena kwa kuwa alishamwomba Mungu na sasa amesamehe kabisa.
Tofauti za wawili hao hazijawahi kutolewa hadharani licha ya mitandao mbalimbali kuzungumzia kuharibika kwa uhusiano wao ikinukuu habari kutoka vikao vya ndani vya Chadema.
Hata hivyo, mapema mwaka huu, Zitto alirushiwa tuhuma nzito na Chadema kutokana na uhusiano wake na baadhi ya makada wa CCM, lakini mbunge huyo aliyahusisha maneno hayo na mwenyekiti wake na aliandika maneno makali dhidi ya Mbowe kwenye ukurasa wake wa facebook.
Lakini katika mahojiano na Mwananchi yaliyofanyika wiki iliyopita nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam, Zitto alionekana kujutia kuharibika huko kwa uhusiano wao na kusema “wapambe ndiyo wanatugombanisha”.
“Sina shida yoyote na Mbowe, naamini ipo siku tutagundua wapambe walituathiri na ndiyo waliotufikisha hapa,” alisisitiza Zitto bila kutaja ni kina nani hasa.
Zitto alisema yeye na Mbowe wametoka mbali tangu akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na hafurahii uhusiano wao ukiishia katika hali hiyo.
“Naumia sana, lakini naamini ipo siku ama nikiwa hai au nimekufa watu wataujua ukweli,” alisema mwanasiasa huyo kijana aliyepata umaarufu kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja.
Alisema, akiwa mwenyekiti wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu (Daruso) yeye na mwenyekiti wake ndiyo waliokijenga chama wakati huo Mbowe akiwa mbunge wa Hai.
Alisema wakati huo Mbowe alikuwa akienda chumbani kwake kusuka mikakati ya kuiinua Chadema na kwamba walikuwa wakila chips pamoja na wakati mwingine kwenye klabu ya usiku ya Bilicanas inayomilikiwa na Mbowe.
“Wakati mwingine naangalia, naumia sana. Wakati tunafanya hayo yote wengine walikuwa CCM, wengine walikuwa wafanyabiashara, lakini sasa ndiyo wana sauti katika chama,” alisema Zitto.
Zitto alisema kuwa wakati huo walikuwa na kampeni yao waliyoiita ‘Real Madrid’ ambayo ilikuwa na lengo la kuingiza kila mwanasiasa bora katika chama chao.
****MWANANCHI***
Tuesday, 29 April 2014
MASHABIKI WA CHELSEA NA LIVERPOOL WALIVYO PIGANA
Pata hiyo na ukome: Shabiki wa Liverpool akimchapa konde wa Chelsea nje ya Uwanja wa Anfield
VURUGU ilizotokea nje ya Uwanja wa Anfield kufuatia Liverpool kufungwa na Chelsea mabao 2-0 jana.
Picha zinaonyesha kitimutimu cha maana nje ya Uwanja wa Anfield Road
baada ya mashabiki wa Liverpool kuwavaa mashabiki wa Chelsea waliokuwa
wakiimba jina la Nahodha wa Wekundu hao, Steven Gerrard baada ya mechi.
Shabiki mmoja alitupa konde kwa mwenzake, wakati wengine walitenganishwa na Polisi.
Makosa ya Gerrard yalisababisha bao la kwanza la Chelsea lililofungwa
na Demba Ba na mashabiki wa The Blues wakawatia hasira Liverpool kwa
kuimba jina la mchezaji huyo.


Mashabiki wakizipiga chanzo ni kuzomewa kwa Steven Gerrard

Polisi wakituliza ghasia

Baba akiongozana na kijana wake kutoka eneo la vurugu huku watu wakiendelea kuchapana nyuma yake

Polisi walilazimika kuwaachanisha watu wengine waliopelekana hadi chini katika mapambano yao

Polisi wakiwwka uzio baina ya mashabiki wa Liverpool na Chelsea

Mashabiki wa Liverpool wakisema na Polisi waliokuwa wakituliza ghasia hizo.
Credit:Matukio na Vijana
KINGUNGE AZUNGUMZA KUHUSU JAJI WARIOBA
Kwanza kabisa nimshukuru Mungu kwa kunipa uzima siku hii ya leo na nikaweza kuandika haya unayoyasoma.
Wiki iliyopita nilimsikiliza kwa makini sana mkongwe wa siasa nchini, mzee Kingunge Ngombale Mwiru alipokuwa akitoa mchango wake katika Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.
Kabla ya kusimama na kuongea, mzee Kingunge nilikuwa najiuliza ni nani wa kutuliza hiki anachofanyiwa Jaji Joseph Sinde Warioba kwa sababu alichokifanya siyo chake binafsi bali ni cha tume na yeye alikuwa ni kiongozi tu.
Haipendezi hata kidogo kuona mjumbe wa bunge anamuambia Jaji wa Warioba afunge mdomo! Hii si haki hata kidogo na siyoheshima.
Mzee Kingunge hakumung’unya maneno alisema wazi kuwa kumtukana au kumshambulia mzee huyo au wajumbe wa tume yake ni sawa na kukitukana Chama Cha Mapinduzi, bila shaka kada huyo alisema hivyo kwa sababu wajumbe wa tume ya kuratibu rasimu ya katiba waliteuliwa na mwenyekiti wa chama ambaye pia ni rais wa nchi.
Akaweka wazi kuwa hatakubali hata kidogo kuona wajumbe wa bunge maalum wakitumia misimamo ya vyama vyao kumshambulia Jaji Warioba au wajumbe wa tume aliyokuwa akiiongoza kwa sababu wanaomshambulia wanaonesha utovu mkubwa wa adabu kwa kuwa chama kina maadili na adabu katika kushughulikia mambo mbalimbali.
Wakati
mzee Kingunge akisema hayo naye Jaji Warioba aliyekuwa Mwenyekiti wa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ameuliza maswali saba ya msingi kwa
wajumbe wa Bunge la Katiba wanaopinga Rasimu ya Katiba waliyoikabidhi
iliyotolewa na tume yake akitaka wawajibu wananchi ili kutuliza kiu yao.
Jaji Warioba ambaye tangu awasilishe Rasimu ya Katiba Desemba 30, mwaka jana amegeuka kuwa adui kwa watu wanaotaka muundo wa serikali mbili, aliuliza maswali hayo katika uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza kuhusu mchakato wa Katiba ambapo alisema:
“Kwanza, jibuni kwa nini mnapinga muundo wa muungano wakati walioupendekeza ni wananchi? Sheria inasema uwepo muungano na mapendekezo katika rasimu hayasemi muungano usiwepo.
Kumbukeni kuwa wananchi walitakiwa kutoa mapendekezo ya namna ya kuuboresha.”Katika swali lake la pili, Warioba alisema kwa nini Tanganyika imevaa koti la muungano? Kwa kuwa katika ukusanyaji wa maoni wananchi walieleza kuwa Serikali ya Muungano wa Tanzania ya sasa siyo ya muungano, ni ya Tanganyika.
Katika swali la tatu alisema wajumbe hao wanatakiwa kujibu maelezo ya wananchi ambao waliieleza tume hiyo kuwa katiba imevunjwa na madaraka ya rais yamechukuliwa na sasa kuna marais wawili katika nchi moja.
“Tume inapewa lawama kubwa, wajibuni wananchi hii tume ilitumwa na nani kukusanya maoni ya wananchi? Waambieni ilikusanya maoni hayo kwa kutumia sheria ipi zaidi ya ile ya Mabadiliko ya Katiba?” alisema Jaji Warioba katika swali lake la nne.
Katika swali lake la tano, Warioba aliwataka wajumbe hao kutoa sababu za kumtuhumu kuwa amependekeza muundo wa serikali tatu kwa sababu yeye pamoja na Joseph Butiku walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji Kisanga na Jaji Nyalali ambazo nazo zilipendekeza muundo wa serikali tatu, kitu ambacho alisema si kweli na hawakuwahi kuwa mjumbe wa tume hizo.
Pia, aliwataka wajumbe hao kujibu swali la sita, kwa nini hawataki kuzungumzia yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na badalayake wanageuza rasimu hiyo kuwa imeandikwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Katika swali lake la saba, aliwataka wajumbe kujibu kwa nini wanaishutumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa imeingiza maoni yake, wakati ilikusanya maoni hayo kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba?
Nilisikiliza kwa makini mijadala ndani ya bunge na kugundua kuwa badala ya kujadili hoja za msingi,
wajumbe wa bunge hilo walikuwa wakitoa lugha za kejeli na matusi kwa baadhi ya watu, kitendo ambacho kwangu mimi naona si sahihi na kinaweza kuligawa taifa kwa sababu yaliyomo katika Rasimu ya Katiba yametokana na maoni ya baadhi ya wananchi.
Siamini kabisa kuwa wajumbe wa tume alijitungia kile kilichoandikwa kwenye rasimu. Siyo hoja hata kidogo kutaja mabaya ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba watafakari na kuboresha rasimu na kamwe wasitumie nafasi yao kujadili watu. Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
Wiki iliyopita nilimsikiliza kwa makini sana mkongwe wa siasa nchini, mzee Kingunge Ngombale Mwiru alipokuwa akitoa mchango wake katika Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.
Kabla ya kusimama na kuongea, mzee Kingunge nilikuwa najiuliza ni nani wa kutuliza hiki anachofanyiwa Jaji Joseph Sinde Warioba kwa sababu alichokifanya siyo chake binafsi bali ni cha tume na yeye alikuwa ni kiongozi tu.
Haipendezi hata kidogo kuona mjumbe wa bunge anamuambia Jaji wa Warioba afunge mdomo! Hii si haki hata kidogo na siyoheshima.
Mzee Kingunge hakumung’unya maneno alisema wazi kuwa kumtukana au kumshambulia mzee huyo au wajumbe wa tume yake ni sawa na kukitukana Chama Cha Mapinduzi, bila shaka kada huyo alisema hivyo kwa sababu wajumbe wa tume ya kuratibu rasimu ya katiba waliteuliwa na mwenyekiti wa chama ambaye pia ni rais wa nchi.
Akaweka wazi kuwa hatakubali hata kidogo kuona wajumbe wa bunge maalum wakitumia misimamo ya vyama vyao kumshambulia Jaji Warioba au wajumbe wa tume aliyokuwa akiiongoza kwa sababu wanaomshambulia wanaonesha utovu mkubwa wa adabu kwa kuwa chama kina maadili na adabu katika kushughulikia mambo mbalimbali.
Wakati
mzee Kingunge akisema hayo naye Jaji Warioba aliyekuwa Mwenyekiti wa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ameuliza maswali saba ya msingi kwa
wajumbe wa Bunge la Katiba wanaopinga Rasimu ya Katiba waliyoikabidhi
iliyotolewa na tume yake akitaka wawajibu wananchi ili kutuliza kiu yao.Jaji Warioba ambaye tangu awasilishe Rasimu ya Katiba Desemba 30, mwaka jana amegeuka kuwa adui kwa watu wanaotaka muundo wa serikali mbili, aliuliza maswali hayo katika uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza kuhusu mchakato wa Katiba ambapo alisema:
“Kwanza, jibuni kwa nini mnapinga muundo wa muungano wakati walioupendekeza ni wananchi? Sheria inasema uwepo muungano na mapendekezo katika rasimu hayasemi muungano usiwepo.
Kumbukeni kuwa wananchi walitakiwa kutoa mapendekezo ya namna ya kuuboresha.”Katika swali lake la pili, Warioba alisema kwa nini Tanganyika imevaa koti la muungano? Kwa kuwa katika ukusanyaji wa maoni wananchi walieleza kuwa Serikali ya Muungano wa Tanzania ya sasa siyo ya muungano, ni ya Tanganyika.
Katika swali la tatu alisema wajumbe hao wanatakiwa kujibu maelezo ya wananchi ambao waliieleza tume hiyo kuwa katiba imevunjwa na madaraka ya rais yamechukuliwa na sasa kuna marais wawili katika nchi moja.
“Tume inapewa lawama kubwa, wajibuni wananchi hii tume ilitumwa na nani kukusanya maoni ya wananchi? Waambieni ilikusanya maoni hayo kwa kutumia sheria ipi zaidi ya ile ya Mabadiliko ya Katiba?” alisema Jaji Warioba katika swali lake la nne.
Katika swali lake la tano, Warioba aliwataka wajumbe hao kutoa sababu za kumtuhumu kuwa amependekeza muundo wa serikali tatu kwa sababu yeye pamoja na Joseph Butiku walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji Kisanga na Jaji Nyalali ambazo nazo zilipendekeza muundo wa serikali tatu, kitu ambacho alisema si kweli na hawakuwahi kuwa mjumbe wa tume hizo.
Pia, aliwataka wajumbe hao kujibu swali la sita, kwa nini hawataki kuzungumzia yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na badalayake wanageuza rasimu hiyo kuwa imeandikwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Katika swali lake la saba, aliwataka wajumbe kujibu kwa nini wanaishutumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa imeingiza maoni yake, wakati ilikusanya maoni hayo kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba?
Nilisikiliza kwa makini mijadala ndani ya bunge na kugundua kuwa badala ya kujadili hoja za msingi,
wajumbe wa bunge hilo walikuwa wakitoa lugha za kejeli na matusi kwa baadhi ya watu, kitendo ambacho kwangu mimi naona si sahihi na kinaweza kuligawa taifa kwa sababu yaliyomo katika Rasimu ya Katiba yametokana na maoni ya baadhi ya wananchi.
Siamini kabisa kuwa wajumbe wa tume alijitungia kile kilichoandikwa kwenye rasimu. Siyo hoja hata kidogo kutaja mabaya ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba watafakari na kuboresha rasimu na kamwe wasitumie nafasi yao kujadili watu. Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
Monday, 28 April 2014
JINSI MAGEREZA WANAVYOPAMBANA NA WAFINGWA WAKOROFI
'Wafungwa' wakijifua kupambana na askari Magereza katika moja ya
maonesho yaliyotia fora sana kwenye sherehe za miaka 50 ya Muungano
katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo

Askari akipambana na 'Mahabusu' aliyeasi


Askari anapangua teke....

Kisha anakata zote bee....

Mfungwa hoi...

Anadakwa kilaaiiini....
Hii ilikuwa ni igizo tu, kwani hakukuwepo na mfungwa halisi bali
askari waliovalia aina ya nguo za wafungwa....Chanzo Michuzi Blog
UKAWA KUSIMAMISHA MGOMBEA MMOJA URAISI 2015
Dar es Salaam. Vyama vinavyounda Umoja wa
Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimeanza maandalizi ya kushirikiana katika
Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya
urais, gazeti hili limebaini.
Kadhalika, vyama hivyo ambavyo ni Chadema, NCCR
Mageuzi na CUF vinakusudia kuwa na mgombea mmoja wa nafasi za wabunge na
madiwani, ikiwa ni hatua ya kuzikabili nguvu za chama tawala, CCM.
Habari zilizolifikia gazeti hili zinasema tayari
viongozi wakuu wa vyama hivyo wamekubaliana kuanza mchakato huo na
wameandika mapendekezo na kuyapeleka katika sekretarieti za vyama vyao
kwa ajili ya kufanyiwa uchambuzi.
Chanzo chetu kilidokeza kuwa kamati ya wataalamu
kutoka vyama hivyo tayari imeundwa ili kuandaa taratibu zitakazotumika
katika kufanikisha mkakati huo.
Wenyeviti wa vyama hivyo walipoulizwa kwa nyakati
tofauti kuhusu mpango huo hawakukubali moja kwa moja, badala yake
walisema ni mapema mno kuzungumzia suala hilo katika vyombo vya habari.
Ukawa ni umoja ambao uliviunganisha vyama vyenye
malengo yanayofanana katika Bunge Maalumu la Katiba na vimekuwa
vikishinikiza kuzingatiwa kwa mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya
Katiba hususan muundo wa Muungano wenye serikali tatu, tofauti na
serikali mbili za sasa.
Umoja huo pia uliwaongoza wajumbe wa Bunge Maalumu
ambao ni wanachama wake kutoka nje kususia mchakato wa Katiba Mpya
kutokana na kile walichodai kuwa ni kutokuridhishwa na jinsi mambo
yanavyokwenda.
Taarifa za kuwapo kwa mpango wa kushirikiana
katika Uchaguzi Mkuu ujao, zimekuja siku chache tangu kufichuliwa kwa
mpango mwingine wa kuundwa upya kwa Baraza la Mawaziri kivuli ambalo
litawajumuisha wabunge wa vyama hivyo katika Bunge la Jamhuri wa
Muungano wa Tanzania.
Baraza la kivuli la sasa linawajumuisha wabunge
kutoka Chadema pekee, ambacho kinaunda Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni
tangu kuanza kwa Bunge la 10, Novemba 2010.
Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Kiongozi wa
Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema atapanga upya baraza
lake katika siku za mwanzo za Bunge la Bajeti, linalotarajiwa kuanza Mei
6, mwaka huu mpango ambao umeungwa mkono na wenyeviti wa CUF na NCCR
Mageuzi.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema
uamuzi huo ni hatua kubwa katika ushirikiano na kwamba tayari
alikwishawaarifu wabunge wa chama chake wawe tayari kushiriki katika
baraza hilo.
<<<<<MWANANCHI>>>>>>>
<<<<<MWANANCHI>>>>>>>
DIAMOND MARUFUKU KUKANYAGA CHINA
STAA wa muziki wa bongo fleva
nchini, Abdul Nassib "Diamond" ametakiwa kutokanyaga kabisa
nchini China na kwamba akitokeza pua yake nchini humo asahau
kabisa kurudi uraiani...
Hiyo inafuatia kijana mmoja mtanzania kukamatwa wiki iliyopita uwanja wa ndege wa Macau China na kudai kuwa yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania....
Habari kutoka Macau China zinadai kuwa kijana huyo aliyejulikana kwa jina moja la Manyota alikamatwa akiwa kwenye harakati za kuingiza mzigo huo wa dawa za kulevya kwa kupitia uwanja wa ndege wa Macau....
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, inaarifiwa kuwa Manyota alikamatwa Alhamisi ya wiki iliyopita katika uwanja uleule aliokamatwa mtanzania mwingine Jackline Patrick, anayesotea rumande mpaka hii leo huko huko Macau China.....
Kijana mmoja wa kitanzania anayefanya shughuli zake huko China amedai kuwa Manyota alikamatwa na maofisa wa usalama wa uwanja wa ndege na katika utetezi wake alidai kuwa yeye ni mwanamuziki toka Afrika Mashariki...
Mtanzania huyo aliendelea kudai kuwa, Manyota baada ya kukamatwa alianza kubabaika kwa kujifanya mwanamuziki na baadae akadai kuwa yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania....
"Alijifanya yeye ni mwanamuziki, baadae akabadilika na kudai yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania na kwamba ndani ya ule mzigo alikuwa hajui kuna nini zaidi ya kuombwa na jamaa zake wa Dar awapelekee nchini China"...Alisema mtanzania huyo
Inasemekana kuwa, ili kujiridhisha, maofisa hao wa usalama wa uwanja wa ndege walimtaka kijana huyo aoneshe moja ya kazi zake na yeye akaishia kuwaonesha moja ya video za Diamond kupitia mtandaoni na kumuonesha mmoja wa wacheza shoo wa mwanamuziki huyo kuwa ndo yeye Manyota...
Inasemekana kuwa, pamoja na utetezi wake huo ambao unaweza kumuingiza matatani Diamond,maofisa hao wa usalama walishndwa kumuelewa na kumtupa ndani.....
Mtanzania huyo alihitimisha kwa kudai kuwa, kutokana na mazingira yalivyo,ni vyema mwanamuzi Diamond akawa makini sana kama atakuwa na safari za kwenda China kwani kwa namna moja ama nyingine jina lake limewekwa kwenye orodha ya majina machafu na wanaweza kumkamata kwa lengo la kuujua ukweli...
Hiyo inafuatia kijana mmoja mtanzania kukamatwa wiki iliyopita uwanja wa ndege wa Macau China na kudai kuwa yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania....
Habari kutoka Macau China zinadai kuwa kijana huyo aliyejulikana kwa jina moja la Manyota alikamatwa akiwa kwenye harakati za kuingiza mzigo huo wa dawa za kulevya kwa kupitia uwanja wa ndege wa Macau....
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, inaarifiwa kuwa Manyota alikamatwa Alhamisi ya wiki iliyopita katika uwanja uleule aliokamatwa mtanzania mwingine Jackline Patrick, anayesotea rumande mpaka hii leo huko huko Macau China.....
Kijana mmoja wa kitanzania anayefanya shughuli zake huko China amedai kuwa Manyota alikamatwa na maofisa wa usalama wa uwanja wa ndege na katika utetezi wake alidai kuwa yeye ni mwanamuziki toka Afrika Mashariki...
Mtanzania huyo aliendelea kudai kuwa, Manyota baada ya kukamatwa alianza kubabaika kwa kujifanya mwanamuziki na baadae akadai kuwa yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania....
"Alijifanya yeye ni mwanamuziki, baadae akabadilika na kudai yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania na kwamba ndani ya ule mzigo alikuwa hajui kuna nini zaidi ya kuombwa na jamaa zake wa Dar awapelekee nchini China"...Alisema mtanzania huyo
Inasemekana kuwa, ili kujiridhisha, maofisa hao wa usalama wa uwanja wa ndege walimtaka kijana huyo aoneshe moja ya kazi zake na yeye akaishia kuwaonesha moja ya video za Diamond kupitia mtandaoni na kumuonesha mmoja wa wacheza shoo wa mwanamuziki huyo kuwa ndo yeye Manyota...
Inasemekana kuwa, pamoja na utetezi wake huo ambao unaweza kumuingiza matatani Diamond,maofisa hao wa usalama walishndwa kumuelewa na kumtupa ndani.....
Mtanzania huyo alihitimisha kwa kudai kuwa, kutokana na mazingira yalivyo,ni vyema mwanamuzi Diamond akawa makini sana kama atakuwa na safari za kwenda China kwani kwa namna moja ama nyingine jina lake limewekwa kwenye orodha ya majina machafu na wanaweza kumkamata kwa lengo la kuujua ukweli...
NIPO TAYARI KUFA KWA AJILI YA DIAMOND
DADA wa hiyari wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Halima Kimwana amejichora tatuu ya jina la staa huyo na kudai anampenda na yupo tayari kufa kwa ajili yake.
Alisema ukaribu wake ni wa kawaida lakini yupo tayari kufa badala yake (Diamond).
“Nipo tayari kufa kwa ajili ya Diamond, nimechora tatuu ya jina lake mkononi kuonesha msisitizo, namkubali” alisema Halima.
DALILI ZA MWISHO WA DUN IA
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship (FGBF)
lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam, Zakaria Kakobe ameibuka na
kuweka wazi kuwa kuonekana kwa Mwezi Mwekundu (Blood Moon), Aprili 15,
mwaka huu ni ishara kuu ya mwisho wa dunia kama maandiko yanavyosema
katika Matendo 2:17-21, Uwazi linakumegea kwa kina.
Askofu Kakobe aliyasema hayo juzi kufuatia tukio hilo lililojiri siku
tano kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo mwezi wote ulipatwa (lunar
eclipse) na kuwa mwekundu kama damu, tukio ambalo pia litatokea tena
mwakani.Kufuatia tukio hilo lenye kuogofya,…
NA WAANDISHI WETU
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship (FGBF) lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam, Zakaria Kakobe ameibuka na kuweka wazi kuwa kuonekana kwa Mwezi Mwekundu (Blood Moon), Aprili 15, mwaka huu ni ishara kuu ya mwisho wa dunia kama maandiko yanavyosema katika Matendo 2:17-21, Uwazi linakumegea kwa kina.
Askofu
Kakobe aliyasema hayo juzi kufuatia tukio hilo lililojiri siku tano
kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo mwezi wote ulipatwa (lunar eclipse) na
kuwa mwekundu kama damu, tukio ambalo pia litatokea tena
mwakani.Kufuatia tukio hilo lenye kuogofya, baadhi ya mitandao ya
kijamii duniani kote imekumbushia maneno ya manabii mbalimbali lakini
zaidi kutoka kwenye Biblia wakisema mwisho wa dunia sasa ni dhahiri.
MSIKIE KWA UNDANI
“Kinachotakiwa kwa watu sasa ni kuacha maovu na kumrudia Mungu. Ni wajibu wa kila mtu kujiweka tayari kwa kuokoka kwani bila kufanya hivyo watakaokutwa katika dhambi watatupwa jehanamu,” alitahadharisha Askofu Kakobe.
Aliongeza kuwa, dalili zote za mwisho wa dunia zilizotajwa katika Biblia ziko wazi kwa sasa, kama vile hilo la mwezi wa damu, kuzuka kwa manabii wa uongo, vita ya nchi na nchi na ukoo kwa ukoo lakini akasema hajui ni kwa nini watu hawataki kuokoka.
NAYE MAMA RWAKATARE
Naye Mchugaji wa Kanisa la Assemblies of God ‘Mikocheni B’ la jijini Dar, Mama Getrude Rwakatare alikiri kulijua hilo la mwezi kuwa wa damu na kusema katiba Biblia, Luka 21:25 Mungu amefafanua kuwa kuna dalili mbalimbali zitajitokeza siku za mwisho wa dunia na sasa zinaanza kuonekana, akawataka watu kuomba bila kuchoka.
“Dalili nyingine ni mataifa kupigana, upendo wa wengi kupoa, manabii wa uongo kuibuka na kadhalika. Haya tunayaona sasa, hivyo watu wote tumrudie Mungu,” alisema Mama Rwakatare.
NABII SUGUYE PIA
Uwazi lilibahatika kuzungumza na Nabii Nicolaus Suguye wa Kanisa la Huduma na Neno la Upatanisho ambaye alisema dalili za mwisho wa dunia ni nyingi ambazo ni mataifa kupigana, kukosa uhusiano mzuri na kuzuka kwa manabii wa uongo.
NABII GEODAVIE AJUAVYO YEYE
Uwazi lilikwenda mbele zaidi kwa kuzungumza na kiongozi wa Kanisa la Ngurumo za Upako lenye makao makuu jijini Arusha, George David ‘GeoDavie’ ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Suala la kupatwa kwa mwezi na kuwa damu ni ishara ya mwisho wa dunia lakini nasisitiza kuwa pia ni jambo la kisayansi zaidi.”
Alizidi kusema kuwa kilichoandikwa kwenye Biblia, Luka 21:25 (Tena kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota na katika nchi, dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake) lazima kikubalike na kila anayemwamini Mungu.
IMANI MWAKYOMA WA TAG
Mchungaji Imani Mwakyoma wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Magomeni jijini Dar, yeye alisema kupatwa kwa mwezi na kuonekana wa rangi ya damu ni mafundisho ambayo watumishi wa Mungu wamekuwa wakiihubiri kila kukicha.
“Tumekuwa tukihubiri kwa muda wa miaka kumi sasa kwamba mwisho utafika pale tu ishara ya anga itakapoanza kuonekana, mwezi kuwa wa damu na jua kuwa giza, siku hizi kila mara jua linapatwa na kuwa giza, bado nini sasa hapo? Watu wamrejee Mungu,” alisema Mchungaji Mwakyoma.
ASKOFU MALASUSA, KARDINALI PENGO
Baadhi ya waumini wa kanisa la Romani Katoliki linaloongozwa na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo na Kanisa la KKT linaloongozwa na Askofu Dr. Alex Gerhaz Malasusa, walisema watumishi hao wa Mungu mara kwa mara wamekuwa wakihubiri watu kutubu kwa kuwa siku za mwisho wa dunia zipo dhahiri kwa sasa.
MCHUNGAJI WA MAREKANI
Naye John Hagee, Mchungaji wa Kanisa la Cornerstone, San Antonio, Texas Marekani na mwanzilishi wa muunganiko wa Wakristo nchini Israeli alishawahi kutoa kitabu akiongozwa na taasisi ya uchunguzi wa anga za juu ya nchi hiyo, NASA kwa kufanya makadirio kupitia historia ambapo aliandika uhusiano wa moja kwa moja kati ya kupatwa kwa mwezi na kuwa mwekundu na utabiri wa Waisrael na wanadamu wote.
NI KARIBU NA PASAKA TU?
Katika kitabu hicho, Mchungaji Hagee aliandika kwamba, zaidi ya miaka 500 iliyopita kupatwa kwa mwezi wa damu kulitokea siku ya kwanza ya Sikukuu ya Pasaka mara tatu tofauti.'
Hata Aprili mwaka huu, mwezi huo ulipatwa na kuwa mwekundu kuelekea Sikukuu ya Pasaka na itatokea tena mwakani kipindi cha Pasaka.
LAZIMA WATU WAJUE ISHARA
Mchungaji Hagee alifafanua kwamba kupatwa kwa mwezi ni lazima watu, hasa Wakristo waelewe ishara hizo. Alisema katika Biblia, Joel: 2 na Matendo ya Mitume: 2 vyote vimeandika tukio hilo kwamba ndiyo mapito ya dunia kuelekea mwisho wake.
BAADA YA MATUKIO HAYA
Kwa mujibu wa Markell, mchambuzi wa mambo ya sayansi, kupatwa kwa mwezi na kuwa wa damu kutatokea tena katika mpangilio wa Oktoba 8, 2014, Aprili 4, 2015 na Septemba 28, 2015!
IMANI YA KIKRISTO
Hata hivyo, Markell anasema kuwa Wakristo wengi wanaamini maneno ya kale kwamba kupatwa kwa mwezi ni dalili ya ujio wa pili wa Kristo na hivyo kusababisha hofu miongoni mwa wale ambao hawajui maana halisi japo maelezo ya kisayansi yanafafanua jambo hili.
Alisema kimsingi, rangi ya mwezi ni nyekundu ambayo ipo katika anga ya dunia na kama dunia haina anga, moja kwa moja mwezi utafunikwa na giza.
Markell ambaye anaamini kwamba shetani yupo nyuma ya harakati za maendeleo, anasema hakuna mtu anayejua ishara za mwezi lakini alipendekeza kuwa dunia inapaswa kubashiri kwa habari mbaya.
<<<<GPL>>>>
Askofu Kakobe aliyasema hayo juzi kufuatia tukio hilo lililojiri siku
tano kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo mwezi wote ulipatwa (lunar
eclipse) na kuwa mwekundu kama damu, tukio ambalo pia litatokea tena
mwakani.Kufuatia tukio hilo lenye kuogofya,…
NA WAANDISHI WETUASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship (FGBF) lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam, Zakaria Kakobe ameibuka na kuweka wazi kuwa kuonekana kwa Mwezi Mwekundu (Blood Moon), Aprili 15, mwaka huu ni ishara kuu ya mwisho wa dunia kama maandiko yanavyosema katika Matendo 2:17-21, Uwazi linakumegea kwa kina.
Askofu
Kakobe aliyasema hayo juzi kufuatia tukio hilo lililojiri siku tano
kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo mwezi wote ulipatwa (lunar eclipse) na
kuwa mwekundu kama damu, tukio ambalo pia litatokea tena
mwakani.Kufuatia tukio hilo lenye kuogofya, baadhi ya mitandao ya
kijamii duniani kote imekumbushia maneno ya manabii mbalimbali lakini
zaidi kutoka kwenye Biblia wakisema mwisho wa dunia sasa ni dhahiri.MSIKIE KWA UNDANI
“Kinachotakiwa kwa watu sasa ni kuacha maovu na kumrudia Mungu. Ni wajibu wa kila mtu kujiweka tayari kwa kuokoka kwani bila kufanya hivyo watakaokutwa katika dhambi watatupwa jehanamu,” alitahadharisha Askofu Kakobe.
Aliongeza kuwa, dalili zote za mwisho wa dunia zilizotajwa katika Biblia ziko wazi kwa sasa, kama vile hilo la mwezi wa damu, kuzuka kwa manabii wa uongo, vita ya nchi na nchi na ukoo kwa ukoo lakini akasema hajui ni kwa nini watu hawataki kuokoka.
NAYE MAMA RWAKATARE
Naye Mchugaji wa Kanisa la Assemblies of God ‘Mikocheni B’ la jijini Dar, Mama Getrude Rwakatare alikiri kulijua hilo la mwezi kuwa wa damu na kusema katiba Biblia, Luka 21:25 Mungu amefafanua kuwa kuna dalili mbalimbali zitajitokeza siku za mwisho wa dunia na sasa zinaanza kuonekana, akawataka watu kuomba bila kuchoka.
“Dalili nyingine ni mataifa kupigana, upendo wa wengi kupoa, manabii wa uongo kuibuka na kadhalika. Haya tunayaona sasa, hivyo watu wote tumrudie Mungu,” alisema Mama Rwakatare.
NABII SUGUYE PIA
Uwazi lilibahatika kuzungumza na Nabii Nicolaus Suguye wa Kanisa la Huduma na Neno la Upatanisho ambaye alisema dalili za mwisho wa dunia ni nyingi ambazo ni mataifa kupigana, kukosa uhusiano mzuri na kuzuka kwa manabii wa uongo.
NABII GEODAVIE AJUAVYO YEYE
Uwazi lilikwenda mbele zaidi kwa kuzungumza na kiongozi wa Kanisa la Ngurumo za Upako lenye makao makuu jijini Arusha, George David ‘GeoDavie’ ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Suala la kupatwa kwa mwezi na kuwa damu ni ishara ya mwisho wa dunia lakini nasisitiza kuwa pia ni jambo la kisayansi zaidi.”
Alizidi kusema kuwa kilichoandikwa kwenye Biblia, Luka 21:25 (Tena kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota na katika nchi, dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake) lazima kikubalike na kila anayemwamini Mungu.
IMANI MWAKYOMA WA TAG
Mchungaji Imani Mwakyoma wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Magomeni jijini Dar, yeye alisema kupatwa kwa mwezi na kuonekana wa rangi ya damu ni mafundisho ambayo watumishi wa Mungu wamekuwa wakiihubiri kila kukicha.
“Tumekuwa tukihubiri kwa muda wa miaka kumi sasa kwamba mwisho utafika pale tu ishara ya anga itakapoanza kuonekana, mwezi kuwa wa damu na jua kuwa giza, siku hizi kila mara jua linapatwa na kuwa giza, bado nini sasa hapo? Watu wamrejee Mungu,” alisema Mchungaji Mwakyoma.
ASKOFU MALASUSA, KARDINALI PENGO
Baadhi ya waumini wa kanisa la Romani Katoliki linaloongozwa na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo na Kanisa la KKT linaloongozwa na Askofu Dr. Alex Gerhaz Malasusa, walisema watumishi hao wa Mungu mara kwa mara wamekuwa wakihubiri watu kutubu kwa kuwa siku za mwisho wa dunia zipo dhahiri kwa sasa.
MCHUNGAJI WA MAREKANI
Naye John Hagee, Mchungaji wa Kanisa la Cornerstone, San Antonio, Texas Marekani na mwanzilishi wa muunganiko wa Wakristo nchini Israeli alishawahi kutoa kitabu akiongozwa na taasisi ya uchunguzi wa anga za juu ya nchi hiyo, NASA kwa kufanya makadirio kupitia historia ambapo aliandika uhusiano wa moja kwa moja kati ya kupatwa kwa mwezi na kuwa mwekundu na utabiri wa Waisrael na wanadamu wote.
NI KARIBU NA PASAKA TU?
Katika kitabu hicho, Mchungaji Hagee aliandika kwamba, zaidi ya miaka 500 iliyopita kupatwa kwa mwezi wa damu kulitokea siku ya kwanza ya Sikukuu ya Pasaka mara tatu tofauti.'
Hata Aprili mwaka huu, mwezi huo ulipatwa na kuwa mwekundu kuelekea Sikukuu ya Pasaka na itatokea tena mwakani kipindi cha Pasaka.
LAZIMA WATU WAJUE ISHARA
Mchungaji Hagee alifafanua kwamba kupatwa kwa mwezi ni lazima watu, hasa Wakristo waelewe ishara hizo. Alisema katika Biblia, Joel: 2 na Matendo ya Mitume: 2 vyote vimeandika tukio hilo kwamba ndiyo mapito ya dunia kuelekea mwisho wake.
BAADA YA MATUKIO HAYA
Kwa mujibu wa Markell, mchambuzi wa mambo ya sayansi, kupatwa kwa mwezi na kuwa wa damu kutatokea tena katika mpangilio wa Oktoba 8, 2014, Aprili 4, 2015 na Septemba 28, 2015!
IMANI YA KIKRISTO
Hata hivyo, Markell anasema kuwa Wakristo wengi wanaamini maneno ya kale kwamba kupatwa kwa mwezi ni dalili ya ujio wa pili wa Kristo na hivyo kusababisha hofu miongoni mwa wale ambao hawajui maana halisi japo maelezo ya kisayansi yanafafanua jambo hili.
Alisema kimsingi, rangi ya mwezi ni nyekundu ambayo ipo katika anga ya dunia na kama dunia haina anga, moja kwa moja mwezi utafunikwa na giza.
Markell ambaye anaamini kwamba shetani yupo nyuma ya harakati za maendeleo, anasema hakuna mtu anayejua ishara za mwezi lakini alipendekeza kuwa dunia inapaswa kubashiri kwa habari mbaya.
<<<<GPL>>>>
Tuesday, 22 April 2014
CHADEMA YAENDELEA KUSAMBARATIKA
Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki
Katibu
Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru wadhifa
huo kuanzia Aprili mwaka huu kutokana na mkanganyiko wa uongozi ndani ya chama
hicho.
Mwapiki
amesema amechoshwa na marumbano ya mara kwa mara na meza kuu ndani ya chama hicho
katika ngazi ya wilaya hivyo kudhoofisha juhudi zake za kukijenga chama hicho.
Aidha
Mwampiki amesema viongozi wa chama hicho wamekuwa na marumbano ya mara kwa mara
hivyo yeye kama kiongozi hayupo tayari kuona mambo yanavurugika katika chama
hicho.
Hata hivyo
katika uamuzi aliouchukua Lucas Mwapiki amesema kuwa yeye atabakia kuwa
mwanachama wa chama hicho na Diwani wa Kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.
Amewataka
wanachama wamuelewe hivyo ameona yeye akae pembeni badala ya kuwa na muda
mwingi wa kujadili migogoro ambayo haina tija na kuleta mkanganyiko kwa
wanachama.
LIGI YA WILAYA YA MKINGA YAPAMBA MOTO
Kikosi cha SHIKASHIKA FC kabla ya mechi ya ligi ya wilaya ya mkinga
Kocha Mkuu wa SHIKASHIKA FC ndugu ALEX MWANGA "FERGASON" akitoa maelekezo kwa wachezaji wake kabla ya mechi ya ligi ya wilaya mkinga
Subscribe to:
Comments (Atom)



