Saturday, 6 December 2014

SIMBA INATISHA

SIMBA imefanya usajili mwingine wa kimyakimya baada ya kumsajili mshambuliaji raia wa Gambia.
Mshambuliaji huyo ametajwa kwa jina la Omar Mboob aliyewasili jana usiku kwa Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.
Ingawa viongozi wa Simba hawakuwa wakipokea simu jana, taarifa za uhakika zinaeleza mshambuliaji huyo kinda anatarajia kuanza mazoezi leo na Simba.
“Kweli Simba wamekuja usiku wa jana (juzi) wakampokea mchezaji mmoja na wamesema anatokea Gambia.
“Walikuja na Hiace yao hapa wakampokea na kuondoka naye lakini walifanya mambo yao harakaharaka utafikiri kuna jambo la uficho.“Nilimsikia kiongozi mmoja akitaka waondoke haraka hapa airport kwa kuwa waliwahofia Yanga,” kilieleza chanzo cha uhakika kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa Kamati ya Utendaji ya Simba alipoulizwa jana, alionekana kushangazwa na swali hilo, lakini hakutoa jibu.“Nani kakuambia, mimi sijui lolote. Wamekuambia anatokea nchi gani? Ila ukweli sina habari ndugu yangu,” alisema.
Ila taarifa za uhakika, zinasisitiza mshambuliaji huyo amefichwa na viongozi wa Simba wamekuwa wakifanya siri kubwa kuhakikisha haijulikani.
Lengo ni kuepuka Yanga au klabu nyingine kuingilia kati ili wajaribu kuona kiwango cha mchezaji huyo kutokea katika Jiji la Banjul, Gambia.Iwapo Mgambia huyo atafuzu, basi itakuwa ni hatari kwa Warundi, Amissi Tambwe na Pierre Kwizera kwa kuwa mmoja wao atalazimika kuachia nafasi.SI

CHRISTIAN KUFUNIKA DAR

Stori: Showbiz
WAKATI siku zikizidi kukatika kuelekea Desemba 6, katika ule Usiku wa Nani Kama Mama ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem, jijini Dar ambapo Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’ anatarajiwa kuweka historia mpya ndani ya ukumbi huo.
Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’.
Akipiga stori na Showbiz, Meneja wa Bella, Amiri Marusu aliongelea usiku huo ambao umekuwa gumzo kubwa kwakuwa ni mara ya kwanza kufanyika uzinduzi wa Albamu ya Nani Kama Mama ndani ya Dar Live hivyo Bella amejipanga vya kutosha kwa kuweka historia mpya ukumbini hapo. “Mashabiki wakae mkao wa kusikia ngoma kali zote kama vile Hanitaki Tena, Usilie aliyoimba na Banana Zoro, Msaliti, Nakuhitaji na nyingine kibao ambazo zipo katika albamu hiyo,” alisema Amiri.
Christian Bella ‘Obama’ akipozi.
Bella ambaye alitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kutua katika bendi ya Akudo Impact na kutengeneza ngoma kali kama Walimwengu si Wanadamu, Bomoa Bomoa, Safari Sio Kifo, Yako Wapi Mapenzi na nyingine nyingi. Ametokea kujizolea umaarufu kwa sauti nyingi tofauti kiasi cha kupelekea kutungiwa jina la Mfalme wa Masauti.

Saturday, 11 October 2014

JEMBE KINANA AENDELEA KUVUNJA CHADEMA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akionesha kadi 27 za wananchama wa Chadema  waliokihama chama hicho na kujiunga na CCM kaatika mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Nyololo, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010. Kulia aliyevaa shati jeupe ni aliyekuwa Katibu wa Kata ya Igowole, Josephat Soda ambapo wengine ni miongoni mwa walio kuwa wafuasi wa Chadema.
 Aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Igowole, Joephat Soda akikabidhi bendera ya chama hicho kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya yeye na wenzie 26 kutangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo.
 Kinana akimkabidhi kadi ya CCM, Josephat Soda baada ya kutanga kujiunga na CCM katika mkutano huo.
 Josephat Soda akielezea jinsi alivyoamua kuondoka Chadema na kujiunga na CCM, ambapo alisema amechoka na chama kilichosheheni uongo, ambapo viongozi wa Chadema alidai kuwa walitoa maagizo kuwaakope fedha za  kujengea Mnara wa mwandishi wa habari Marehemu David Mwangosi, aliyeuawa wakati wa vurugu za Chadema na Polisi katika Mji wa Nyololo, ambapo walimuahidi kumtumia fedha zilizotumika kujenga mnara huo ahadi ambayo hadi sasa haalipwa na anadaiwa na muuza simenti na muuza saruji alikokopa. CCM imeamua kulipa madeni yote aliyokuwa akidaiwa.
Wanachama wa CCM wakiwemo wapya kutoka Chadema, wakiapa kiapo cha utii cha CCM baada ya kukabidhiwa kadi wakati wa mkutano huo.
<<<<<<<<GPL>>>>>>>>

JAMBAZI SUGU LAUWAWA ARUSHA

 
Wakazi wa Jiji la Arusha wakiwa katika Kituo cha Polisi mkoani humo kushuhudia mwili wa mtu anayedaiwa kuwa jambazi sugu, Ramadhan Abdallah Jumanne (Rama Ndonga), aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi usiku wa kuamkia jana. Picha na Happy Lazaro.       


Arusha. Jeshi la Polisi mkoani Arusha limefanikiwa kumuua jambazi aliyekuwa akiutikisa mkoa huo kwa matukio ya kuteka na kuwapora wanawake wenye magari na kisha kuwapiga risasi.
Mtu huyo aliyefahamika kwa kwa jina la Ramadhan Abdallah Jumanne maarufu kama Rama Ndonga (37) Mkazi wa Moivo hatimaye ameuawa polisi baada ya kupigwa risasi katika majibizano na askari wa jeshi hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema jambazi huyo aliuawa usiku wa kuamkia jana majira ya saa 2:04 usiku katika Kijiji cha Moivo, Kitongoji cha Enaboishu wilayani Arumeru.
Alisema baadhi ya matukio ya ujambazi aliyowahi kuhusika nayo ni lililotokea Agosti 6 mwaka huu saa 3:30 usiku maeneo ya Kwa Iddi ambapo walimpiga risasi sehemu ya shingo mwanamke Shamimu Rashid aliyekuwa Mkazi wa Sakini wakati akijiandaa kuingia nyumbani kwake na kumuua.
Kamanda Sabas alitaja tukio lingine ni la Agosti 21 mwaka huu majira ya saa 1:00 huko maeneo ya Olasiti, jambazi huyo akiwa na mwenzake kwenye pikipiki walimjeruhi kwa kumpiga risasi ya mdomoni na kutokea kichwani mtoto Christen Nickson mwenye umri wa miaka mitatu na nusu na kisha kufanikiwa kupora Sh200,000 na baadaye majeruhi huyo alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru.
Aidha, kukamatwa kwa jambazi huyo ni baada ya polisi kutumia mbinu za kisasa na kufika nyumbani kwa marehemu na polisi walimwamuru ajisalimishe lakini alikaidi na kuanza kuwarushia risasi hali iliyosababisha askari kujibu mapigo na hatimaye kusababisha kifo chake.
Alisema kuwa, baada ya upekuzi mwili wa marehemu ulipatikana na bastola aina ya Glock 19 yenye namba RLU 976 iliyotengenezwa nchini Australia ikiwa na magazine yenye risasi 14 ambayo alikuwa ameishika mkononi pamoja na maganda matano ya risasi.
Aidha, upekuzi zaidi uliofanywa katika chumba chake ulibaini magazine moja yenye risasi 15 na magazine mbili zenye uwezo wa kubeba risasi 30 kila moja, redio call moja yenye nembo ya ITSS/UNICTR, pikipiki aina ya Toyo Power King rangi nyekundu yenye namba za usajili T 507 BSU.
Upekuzi zaidi ulibaini kofia ngumu ya kuendesha pikipiki rangi nyekundu, plate number ya pikipiki yenye namba T 805 CVD, pingu moja, Glock Fab Defence moja na vifaa vya kusafishia bastola pamoja na koti jeusi.
Kamanda Sabas alisema polisi wanaendelea kumsaka mwenzake waliyekuwa wakitumia naye pikipiki hiyo, ili kuweza kuutokomeza mtandao huo ambao umekuwa tishio jijini Arusha.
Kutokana na tukio hilo, watu walifurika kituo cha polisi kushuhudia mwili wa marehemu ambaye aliutikisa mji huo.

POLICE 120 WATIMULIWA CHUONI MOSHI

 
Moshi. Maofisa wa Polisi wapatao 120 wa Jeshi la Polisi, waliokuwa wakihudhuria mafunzo ya kupandishwa vyeo katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA), wametimuliwa chuoni hapo.
Habari za uhakika zilizopatikana jana kutoka ndani ya chuo hicho zamani kikijulikana kama CCP, zimedai uamuzi wa kuwaondoa chuoni ulitangazwa jana na mkuu wa chuo hicho, Matanga Mbushi.
Vyanzo mbalimbali vililidokeza gazeti hili kuwa, waliotimuliwa chuoni hapo ni maofisa ambao wana ulemavu wa aina mbalimbali walioupata wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi.
Habari hizo zilisema hadi jana saa 9:00 alasiri, maofisa hao walikuwa ofisi za mkuu wa chuo hicho wakisubiri kupatiwa maelekezo ya namna ya kurejea katika vituo vyao vya kazi mikoa mbalimbali.
“Wako 120 hivi walikuja hapa (MPA) kwa ajili ya kuchukua kozi za Koplo, Sajenti, Meja na ‘Assistant Inspector’ (wakaguzi wasaidizi), lakini ndiyo hivyo wametuambia tuondoke,” kilidokeza chanzo chetu.
Hata hivyo, ofisa mmoja alilidokeza gazeti hili kwamba mkuu wa zamani Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, ambaye amestaafu, ndiye wa kulaumiwa kwa kutoheshimu mapendekezo ya wataalamu.
“Tulimwambia IGP Mwema kwamba ni vizuri kama maofisa wenye ulemavu kama baadhi ya vigezo wanavyo basi wapewe vyeo huko huko mikoani, lakini wasiende chuoni,” alidokeza na kuongeza;
“Tulipendekeza yafunguliwe madarasa ya kanda wakishafanya mtihani wa kawaida wapewe vyeo huko huko, lakini wakija chuoni ni lazima wahudhurie vipindi vyote ambavyo vinafanya chuo kiitwe chuo.
“Chuo chochote kile kina vigezo vyake na kwamba ili mtu apate cheo alichokwenda kukisomea ni lazima ahudhurie asimilia 95 ya vipindi ikiwamo kwata, medani za kivita na kuzuia vurugu,”alisema.
Chanzo kingine kililidokeza gazeti hili kuwa maofisa hao waliripoti chuoni hapo wiki mbili zilizopita na katika uchunguzi, walibainika wana ulemavu ambao hawawezi kumudu mafunzo ya ukakamavu.
Mmoja wa maofisa hao waliotimuliwa alilalamika kuwa kitendo hicho siyo cha kiungwana kwa kuwa ulemavu huo waliupata wakiwa kazini wakilitumikia Taifa na hawajashindwa kuingia darasani.
“Baadhi yetu tumefanya kazi miaka 20 wengine 25. Wamekatika miguu. Wako trafiki wamegongwa na polisi wengine wamepigwa risasi na majambazi wakapata ulemavu si sawa kutunyima vyeo,”

Monday, 22 September 2014

SIMBA KAKABWA KOO NA WAGOSI WA KAYA


0
Share

Dar es Salaam. Makosa ya mabeki wa Simba yaliyofanywa dakika za majeruhi, yaliipa sare ya kwanza msimu huu baada ya kufungana 2-2 na Coastal Union ya Tanga katika mechi ya kupendeza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.Katika mchezo huo, Coastal walitumia dakika nane za majeruhi kipindi cha pili kufunga bao la kusawazisha na kuinyima Simba ushindi katika mechi yao ya kwanza msimu huu.Bao la Coastal lilitokana na makosa ya kiufundi ya mabeki wa Simba walioshindwa kuweka ukuta imara kuzuia kiki ya adhabu ndogo iliyopigwa na Ramadhan Salum dakika ya 82 na kwenda moja kwa moja kwenye kamba za Wekundu hao.
Kosa la kwanza lililoigharimu Simba na kuipa Coastal kupata bao la kwanza, lilifanywa na kiungo Pierre Kwizera aliyeshindwa kuumiliki vizuri mpira kabla ya kunaswa na wachezaji wa Coastal Union na Lutimba Yayo Kato kuutumbukiza wavuni kwa kiki ya karibu na lango.
Kwa matokeo ya mchezo wa jana, Simba na Coastal Union zimezoa pointi moja kila mmoja.
Mchezo wa jana uliokamilisha mechi za kwanza za raundi ya kwanza ya ligi hiyo, ulianza kwa Simba kusalimia lango la wapinzani wao na kuandika bao la kwanza kupitia kwa Shaaban Kisiga. Kisiga alifunga bao hilo kwa mpira wa faulo dakika ya saba kabla ya Amis Tambwe kufumania nyavu dakika ya 36 akiunganisha kwa kichwa akimalizia krosi ya Emmanuel Okwi.
Kwa upande mwingine, juhudi za Simba kupata mabao, zilichangiwa kwa kiasi kikubwa na Okwi kwani bao la kwanza, aliangushwa nje ya 18 na beki wa Coastal, Tumba Swedi kabla ya Kisiga kufunga kwa faulo, pia alipiga krosi ambayo iliunganishwa na Tambwe kuandikia bao la pili.Jitihada za Union kusaka bao zilizaa matunda katika dakika ya 67 baada ya Lutimba Yayo Kato kufanikiwa kumtungua kipa wa Simba, Ivo Mapunda kufuatia pande la Itubu.
Ikishambulia mfululizo, Coastal Union ilisawazisha dakika ya 82 kupitia kwa Ramadhan Salum aliyetandika mpira wa faulo uliokwenda moja kwa moja nyavuni.
Simba waliianza mechi ya jana kwa kasi huku wakitawala sehemu ya kiungo, lakini mipira yao ya mwisho haikuwa makini na hivyo kushindwa kutengeneza nafasi za mabao huku Haruna Chanongo akipoteza chache walizozipata.
Katika kipindi cha kwanza, Coastal walitumia muda mwingi kulinda lango zaidi kuliko kushambulia, huku pia ikifanya mashabulizi ya kushtukiza wakimtumia mshambuliaji Itubu Imbem.
Kipindi cha pili, Simba walifanya mabadiliko kwa kuwatoa Chanongo na Tambwe na nafasi zao kuchukuliwa na Uhuru Selemani na Rafael Kiongera, wakati Coastal waliwatoa Seleman Kibuta, Razak Khalfan na Joseph Mahindi na nafasi zao kuchukuliwa na Lutimba Yayo Kato, Ayoub Yahaya na Abbas Athuman.
Mabadiliko hayo yaliwanufaisha Coastal kwani walipata mabao mawili. Akizungumza baada ya mechi kumalizika kocha wa Simba, Patrick Phiri alisema: “Coastal walicheza vizuri, sijafurahia matokeo tuliyoyapata ila tutajiandaa kwa ajili ya mechi ijayo.”

MAN U YABAMIZWA 5

V
London, England. Leicester City ilitoka nyuma kwa mabao 3-1 na kuibuka na ushindi wa mabao 5-3 dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu England uliochezwa jana.
United walionekana kama wangeibuka na ushindi wakati Robin van Persie alipofunga bao la mapema kabla ya Angel Di Maria kufunga la pili, lakini bao la kichwa la Leonardo Ulloa lilifanya matokeo kuwa 2-1 kabla ya Ander Herrera kufunga la tatu kwa United.
Leicester walirudi uwanjani kwa kasi na kupata penalti iliyofungwa na David Nugent na Esteban Cambiasso alisawazisha bao la tatu, wakati Jamie Vardy akifunga la nne kabla ya Ulloa kufunga la tano.
Ikiwatumia washambuliaji watatu, Radamel Falcao, Wayne Rooney na Robin van Persie, United ilishindwa kucheza vizuri katika kipindi cha pili na kuiruhusu Leicister kumiliki mpira walivyotaka.
Bao la Andre Schurrle la kipindi cha pili lilisawazishwa na Frank Lampard na kufanya mchezo kati ya Manchester City na Chelsea kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Vijana wa kocha Jose Mourinho walilazimisha sare hiyo ugenini katika Uwanja wa Etihad na kufikisha pointi 13 kileleni ikiwa na michezo mitano iliyocheza.
Katika mchezo huo, beki wa pembeni wa City, Pablo Zabaleta alitolewa kwa kadi ya pili ya njano kutokana na kumchezea vibaya Diego Costa kipindi cha pili.
Mchezo huo ulionyesha kuwa ungekuwa na kadi nyekundu baada ya wachezaji saba kuonyeshwa kadi za njano katika kipindi cha kwanza. Kwa matokeo hayo, Chelsea imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo ikiwa na tofauti ya pointi tatu, ikifuatiwa na Southamptom wenye pointi 10.

Monday, 8 September 2014

MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA JIMBONI KWAKE


Mh:Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr.Kone wakati wakukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Maabara za  Kisasa Katika Shule za Jimbo la Iramba,Hapa ni Shule ya Kijiji cha Usule.Kufikia Tar.31/09/2014 Mkuu wa Mkoa anategemea Kumkabidhi Mh:Rais Jakaya Kikwete Maabara zote za Shule za Sekondari zikiwa zimekamilika ndani ya Mkoa wa SIngida kuendana na Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.
 Mh:Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa Kijiji cha Usule waliofika kusikiliza mambo mbalimbali ya Utekelezaji wa Shughuli za Maendeleo.Kwaya ya akina mama Kiji cha Usule wakitumbuiza mbele ya Mgeni Rasmi Mh:Mwigulu Nchemba(hayupo pichani).Vijana wakifurahia Ushindi wao katika Michuoano ya MWIGULU CUP,Hii ni timu ya Kijiji cha Usule.Akina mama wakionesha kadi zao za Chama cha Mapinduzi kuonesha kuwa wao bila CCM haiwezekani.Wananchi wakishangilia baada ya Kuona Nguzo za Umme zikipita kijijini kwao Ishara kuwa Umeme umewafikia.
Mh:Mwigulu akimsikiliza Mmoja wa Wazee wa kijiji cha Usule.Mkutano unaendelea huku Mh:Mwigulu nchemba akiwafafanulia mambo mbalimbali ya maendeleo wanakijiji wa Usule,Kubwa ni Usambazaji wa maji hapo Kijijini ambao tayari umekwisha anza,Pia amesisitiza Kusuka nyaya za Umeme wakati huu Umeme unapowekwa kwenye nguzo,Ukiingiza Umeme wakati huu mafundi wakiwa wanasambaza nyaya ni Bei nafuu 27000/= tu.Ilikukamilisha Ujenzi wa Maabara ya Shule ya Usule Mh:Mwigulu amechangia Mifuko 100 ya Sementi na ameagiza kwenye Upungufu wowote Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi atoe taarifa.Hivyo hivyo amesaidia Uchimbaji wa Bwawa la maji kama Mpango wa Muda mfupi wakati Bomba za Maji zikiendelea Kusambazwa kijiji chote cha Usule.Baadhi ya Vijaja Kijiji cha Kibaya wakiwa kwenye Jezi zao za MWIGULU CUP.Mh:Mwigulu Nchemba akikabidhi Mchango wake wa bati 70 kwa Diwani wa kata ya Mbelekesye kwaajili ya kuezeka Madarasa ya shule ya Mbelekesye yaliyoongezwa.Pia amechangia Mifuko 100 na Mbao kwaajili ya kupau madarasa hayo.
Wakati hili likifanyika katika kijiji cha Kibaya,Mh:Mwigulu Nchemba jana alikabidhi Mabati 320 kijiji cha Misuna kwaajili ya Ujenzi wa Zahanati.Wananchi wakibaya wakifurahia na Mbunge wao.

OKWI HURU KUCHEZA SIMBA

Wajumbe wa Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya TFF wakiwa katika mkutano jijini Dar es Salaam jana. Picha na Said Khamis.      
Dar es Salaam. Utata wa Emmanuel Okwi umemalizwa rasmi na mchezaji huyo wa Uganda sasa yupo huru.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilikutana jana na kupitia masuala mbalimbali ikiwamo mgogoro wa kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi.
Mkataba huo ulipitiwa na kamati ikiwamo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na upande wa Yanga na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa mkataba wa pande mbili haupo kwa sababu Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili.
“Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27 mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote,” alisema Wambura.
Alifafanua kuwa mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), ambapo Kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo, hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja.
Pamoja na Yanga kuwasilisha pingamizi la kuwepo mmoja wa wajumbe katika kikao kwa sababu za kimaslahi (conflict of interests), walifahamishwa kuwa kilichopo mbele ya kamati ni mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, na si usajili.
Pia lilijitokeza suala la Okwi kutakiwa na klabu ya Wadi Degla ya Misri.
Kamati imeiagiza Sekretarieti ya TFF kulifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa katika kikao kijacho.
Hata hivyo mjumbe ambaye Yanga ilimpinga hakushiriki katika kuchangia hoja na kutoa maamuzi.
Uamuzi wa kamati ulifanyika baada ya majadiliano, hivyo hakukuwa na suala la kupiga kura.
Kuhusu pingamizi la Coastal Union kwa Abdi Banda, Kamati imebaini kuwa klabu hiyo imevunja mkataba kati ya pande hizo mbili kwa kushindwa kumlipa mchezaji huyo mshahara wa miezi mitatu mfululizo kama takwa la mkataba.

ZITO :ATOA YA MOYONI


Dar es Salaam. Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameeleza tofauti yake na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akisema imesababishwa na watu aliowaita wapambe.
Zitto (37), ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Chadema, alisema kuwa hata kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya chama kulisababishwa na wapambe hao, lakini akasisitiza kuwa hana kinyongo tena kwa kuwa alishamwomba Mungu na sasa amesamehe kabisa.
Tofauti za wawili hao hazijawahi kutolewa hadharani licha ya mitandao mbalimbali kuzungumzia kuharibika kwa uhusiano wao ikinukuu habari kutoka vikao vya ndani vya Chadema.
Hata hivyo, mapema mwaka huu, Zitto alirushiwa tuhuma nzito na Chadema kutokana na uhusiano wake na baadhi ya makada wa CCM, lakini mbunge huyo aliyahusisha maneno hayo na mwenyekiti wake na aliandika maneno makali dhidi ya Mbowe kwenye ukurasa wake wa facebook.
Lakini katika mahojiano na Mwananchi yaliyofanyika wiki iliyopita nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam, Zitto alionekana kujutia kuharibika huko kwa uhusiano wao na kusema “wapambe ndiyo wanatugombanisha”.
“Sina shida yoyote na Mbowe, naamini ipo siku tutagundua wapambe walituathiri na ndiyo waliotufikisha hapa,” alisisitiza Zitto bila kutaja ni kina nani hasa.
Zitto alisema yeye na Mbowe wametoka mbali tangu akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na hafurahii uhusiano wao ukiishia katika hali hiyo.
“Naumia sana, lakini naamini ipo siku ama nikiwa hai au nimekufa watu wataujua ukweli,” alisema mwanasiasa huyo kijana aliyepata umaarufu kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja.
Alisema, akiwa mwenyekiti wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu (Daruso) yeye na mwenyekiti wake ndiyo waliokijenga chama wakati huo Mbowe akiwa mbunge wa Hai.
Alisema wakati huo Mbowe alikuwa akienda chumbani kwake kusuka mikakati ya kuiinua Chadema na kwamba walikuwa wakila chips pamoja na wakati mwingine kwenye klabu ya usiku ya Bilicanas inayomilikiwa na Mbowe.
“Wakati mwingine naangalia, naumia sana. Wakati tunafanya hayo yote wengine walikuwa CCM, wengine walikuwa wafanyabiashara, lakini sasa ndiyo wana sauti katika chama,” alisema Zitto.
Zitto alisema kuwa wakati huo walikuwa na kampeni yao waliyoiita ‘Real Madrid’ ambayo ilikuwa na lengo la kuingiza kila mwanasiasa bora katika chama chao.
****MWANANCHI***

Tuesday, 29 April 2014

MASHABIKI WA CHELSEA NA LIVERPOOL WALIVYO PIGANA

Pata hiyo na ukome: Shabiki wa Liverpool akimchapa konde wa Chelsea nje ya Uwanja wa Anfield
VURUGU ilizotokea nje ya Uwanja wa Anfield kufuatia Liverpool kufungwa na Chelsea mabao 2-0 jana.
Picha zinaonyesha kitimutimu cha maana nje ya Uwanja wa Anfield Road baada ya mashabiki wa Liverpool kuwavaa mashabiki wa Chelsea waliokuwa wakiimba jina la Nahodha wa Wekundu hao, Steven Gerrard baada ya mechi.
Shabiki mmoja alitupa konde kwa mwenzake, wakati wengine walitenganishwa na Polisi.

Makosa ya Gerrard yalisababisha bao la kwanza la Chelsea lililofungwa na Demba Ba na mashabiki wa The Blues wakawatia hasira Liverpool kwa kuimba jina la mchezaji huyo. 
Mashabiki wa Chelsea wakizomea kwa jeuri ya ushindi wa 2-0
Mashabiki wakizipiga chanzo ni kuzomewa kwa Steven Gerrard
Polisi wakituliza ghasia
Baba akiongozana na kijana wake kutoka eneo la vurugu huku watu wakiendelea kuchapana nyuma yake
Polisi walilazimika kuwaachanisha watu wengine waliopelekana hadi chini katika mapambano yao
Polisi wakiwwka uzio baina ya mashabiki wa Liverpool na Chelsea
Mashabiki wa Liverpool wakisema na Polisi waliokuwa wakituliza ghasia hizo.
Credit:Matukio na Vijana

KINGUNGE AZUNGUMZA KUHUSU JAJI WARIOBA

Kwanza kabisa nimshukuru Mungu kwa kunipa uzima siku hii ya leo na nikaweza kuandika haya unayoyasoma.
Wiki iliyopita nilimsikiliza kwa makini sana mkongwe wa siasa nchini, mzee Kingunge Ngombale Mwiru alipokuwa akitoa mchango wake katika Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.
Mzee Kingunge akisisitiza jambo
Kabla ya kusimama na kuongea, mzee Kingunge nilikuwa najiuliza ni nani wa kutuliza hiki anachofanyiwa Jaji Joseph Sinde Warioba kwa sababu alichokifanya siyo chake binafsi bali ni cha tume na yeye alikuwa ni kiongozi tu.
Haipendezi hata kidogo kuona mjumbe wa bunge anamuambia Jaji wa Warioba afunge mdomo! Hii si haki hata kidogo na siyoheshima.
Mzee Kingunge hakumung’unya maneno alisema wazi kuwa kumtukana au kumshambulia mzee huyo au wajumbe wa tume yake ni sawa na kukitukana Chama Cha Mapinduzi, bila shaka kada huyo alisema hivyo kwa sababu wajumbe wa tume ya kuratibu rasimu ya katiba waliteuliwa na mwenyekiti wa chama ambaye pia ni rais wa nchi.
Akaweka wazi kuwa hatakubali hata kidogo kuona wajumbe wa bunge maalum wakitumia misimamo ya vyama vyao kumshambulia Jaji Warioba au wajumbe wa tume aliyokuwa akiiongoza kwa sababu wanaomshambulia wanaonesha utovu mkubwa wa adabu kwa kuwa chama kina maadili na adabu katika kushughulikia mambo mbalimbali.
Wakati mzee Kingunge akisema hayo naye Jaji Warioba aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ameuliza maswali saba ya msingi kwa wajumbe wa Bunge la Katiba wanaopinga Rasimu ya Katiba waliyoikabidhi iliyotolewa na tume yake akitaka wawajibu wananchi ili kutuliza kiu yao.
Jaji Warioba ambaye tangu awasilishe Rasimu ya Katiba Desemba 30, mwaka jana amegeuka kuwa adui kwa watu wanaotaka muundo wa serikali mbili, aliuliza maswali hayo katika uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza kuhusu mchakato wa Katiba ambapo alisema:
“Kwanza, jibuni kwa nini mnapinga muundo wa muungano wakati walioupendekeza ni wananchi? Sheria inasema uwepo muungano na mapendekezo katika rasimu hayasemi muungano usiwepo.
Kumbukeni kuwa wananchi walitakiwa kutoa mapendekezo ya namna ya kuuboresha.”Katika swali lake la pili, Warioba alisema kwa nini Tanganyika imevaa koti la muungano? Kwa kuwa katika ukusanyaji wa maoni wananchi walieleza kuwa Serikali ya Muungano wa Tanzania ya sasa siyo ya muungano, ni ya Tanganyika.
Katika swali la tatu alisema wajumbe hao wanatakiwa kujibu maelezo ya wananchi ambao waliieleza tume hiyo kuwa katiba imevunjwa na madaraka ya rais yamechukuliwa na sasa kuna marais wawili katika nchi moja.
“Tume inapewa lawama kubwa, wajibuni wananchi hii tume ilitumwa na nani kukusanya maoni ya wananchi? Waambieni ilikusanya maoni hayo kwa kutumia sheria ipi zaidi ya ile ya Mabadiliko ya Katiba?” alisema Jaji Warioba katika swali lake la nne.
Katika swali lake la tano, Warioba aliwataka wajumbe hao kutoa sababu za kumtuhumu kuwa amependekeza muundo wa serikali tatu kwa sababu yeye pamoja na Joseph Butiku walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji Kisanga na Jaji Nyalali ambazo nazo zilipendekeza muundo wa serikali tatu, kitu ambacho alisema si kweli na hawakuwahi kuwa mjumbe wa tume hizo.
Pia, aliwataka wajumbe hao kujibu swali la sita, kwa nini hawataki kuzungumzia yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na badalayake wanageuza rasimu hiyo kuwa imeandikwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Katika swali lake la saba, aliwataka wajumbe kujibu kwa nini wanaishutumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa imeingiza maoni yake, wakati ilikusanya maoni hayo kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba?
Nilisikiliza kwa makini mijadala ndani ya bunge na kugundua kuwa badala ya kujadili hoja za msingi,
wajumbe wa bunge hilo walikuwa wakitoa lugha za kejeli na matusi kwa baadhi ya watu, kitendo ambacho kwangu mimi naona si sahihi na kinaweza kuligawa taifa kwa sababu yaliyomo katika Rasimu ya Katiba yametokana na maoni ya baadhi ya wananchi.
Siamini kabisa kuwa wajumbe wa tume alijitungia kile kilichoandikwa kwenye rasimu. Siyo hoja hata kidogo kutaja mabaya ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba watafakari na kuboresha rasimu na kamwe wasitumie nafasi yao kujadili watu. Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

Monday, 28 April 2014

JINSI MAGEREZA WANAVYOPAMBANA NA WAFINGWA WAKOROFI

'Wafungwa' wakijifua kupambana na askari Magereza katika moja ya maonesho yaliyotia fora sana kwenye sherehe za miaka 50 ya Muungano katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo
Askari akipambana na 'Mahabusu' aliyeasi
Askari akila sahani moja na 'wafungwa' watatu
Askari anapangua teke....
Kisha anakata zote bee....
Mfungwa hoi...
Anadakwa kilaaiiini....
Hii ilikuwa ni igizo tu, kwani hakukuwepo na mfungwa halisi bali askari waliovalia aina ya nguo za wafungwa....Chanzo Michuzi Blog

UKAWA KUSIMAMISHA MGOMBEA MMOJA URAISI 2015

Dar es Salaam. Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimeanza maandalizi ya kushirikiana katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya urais, gazeti hili limebaini.
Kadhalika, vyama hivyo ambavyo ni Chadema, NCCR Mageuzi na CUF vinakusudia kuwa na mgombea mmoja wa nafasi za wabunge na madiwani, ikiwa ni hatua ya kuzikabili nguvu za chama tawala, CCM.
Habari zilizolifikia gazeti hili zinasema tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo wamekubaliana kuanza mchakato huo na wameandika mapendekezo na kuyapeleka katika sekretarieti za vyama vyao kwa ajili ya kufanyiwa uchambuzi.
Chanzo chetu kilidokeza kuwa kamati ya wataalamu kutoka vyama hivyo tayari imeundwa ili kuandaa taratibu zitakazotumika katika kufanikisha mkakati huo.
Wenyeviti wa vyama hivyo walipoulizwa kwa nyakati tofauti kuhusu mpango huo hawakukubali moja kwa moja, badala yake walisema ni mapema mno kuzungumzia suala hilo katika vyombo vya habari.
Ukawa ni umoja ambao uliviunganisha vyama vyenye malengo yanayofanana katika Bunge Maalumu la Katiba na vimekuwa vikishinikiza kuzingatiwa kwa mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba hususan muundo wa Muungano wenye serikali tatu, tofauti na serikali mbili za sasa.
Umoja huo pia uliwaongoza wajumbe wa Bunge Maalumu ambao ni wanachama wake kutoka nje kususia mchakato wa Katiba Mpya kutokana na kile walichodai kuwa ni kutokuridhishwa na jinsi mambo yanavyokwenda.
Taarifa za kuwapo kwa mpango wa kushirikiana katika Uchaguzi Mkuu ujao, zimekuja siku chache tangu kufichuliwa kwa mpango mwingine wa kuundwa upya kwa Baraza la Mawaziri kivuli ambalo litawajumuisha wabunge wa vyama hivyo katika Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Baraza la kivuli la sasa linawajumuisha wabunge kutoka Chadema pekee, ambacho kinaunda Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni tangu kuanza kwa Bunge la 10, Novemba 2010.
Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema atapanga upya baraza lake katika siku za mwanzo za Bunge la Bajeti, linalotarajiwa kuanza Mei 6, mwaka huu mpango ambao umeungwa mkono na wenyeviti wa CUF na NCCR Mageuzi.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema uamuzi huo ni hatua kubwa katika ushirikiano na kwamba tayari alikwishawaarifu wabunge wa chama chake wawe tayari kushiriki katika baraza hilo.

<<<<<MWANANCHI>>>>>>>

DIAMOND MARUFUKU KUKANYAGA CHINA


STAA  wa  muziki  wa  bongo  fleva  nchini, Abdul  Nassib  "Diamond"  ametakiwa  kutokanyaga  kabisa  nchini  China  na  kwamba  akitokeza  pua  yake  nchini  humo  asahau  kabisa  kurudi  uraiani...

Hiyo  inafuatia  kijana  mmoja  mtanzania  kukamatwa  wiki  iliyopita  uwanja  wa  ndege  wa   Macau   China  na  kudai  kuwa  yeye  ni  mcheza  shoo  wa  mwanamuziki  Diamond  kutoka  Tanzania....

Habari  kutoka  Macau  China  zinadai  kuwa  kijana  huyo  aliyejulikana  kwa  jina  moja  la  Manyota  alikamatwa  akiwa  kwenye  harakati  za  kuingiza   mzigo  huo  wa  dawa  za  kulevya  kwa  kupitia  uwanja  wa  ndege  wa  Macau....

Kwa  mujibu  wa  vyanzo  vyetu  vya  habari, inaarifiwa  kuwa  Manyota  alikamatwa  Alhamisi  ya  wiki  iliyopita  katika  uwanja  uleule  aliokamatwa  mtanzania  mwingine  Jackline  Patrick, anayesotea  rumande  mpaka  hii  leo  huko  huko  Macau  China.....

Kijana  mmoja  wa  kitanzania  anayefanya  shughuli  zake  huko  China  amedai  kuwa  Manyota  alikamatwa  na  maofisa  wa  usalama  wa  uwanja  wa  ndege  na  katika  utetezi  wake  alidai  kuwa  yeye  ni  mwanamuziki  toka  Afrika  Mashariki...

Mtanzania  huyo  aliendelea  kudai  kuwa, Manyota  baada  ya  kukamatwa  alianza  kubabaika  kwa  kujifanya  mwanamuziki  na  baadae  akadai  kuwa  yeye  ni  mcheza  shoo  wa  mwanamuziki  Diamond  kutoka  Tanzania....

"Alijifanya  yeye  ni  mwanamuziki, baadae  akabadilika  na  kudai  yeye  ni  mcheza  shoo  wa  mwanamuziki  Diamond  kutoka  Tanzania  na  kwamba  ndani  ya  ule  mzigo  alikuwa  hajui  kuna nini  zaidi  ya  kuombwa  na  jamaa  zake  wa  Dar  awapelekee  nchini  China"...Alisema  mtanzania  huyo

Inasemekana  kuwa, ili  kujiridhisha, maofisa  hao  wa  usalama  wa  uwanja wa  ndege    walimtaka  kijana  huyo  aoneshe  moja  ya  kazi  zake  na  yeye  akaishia  kuwaonesha  moja  ya  video  za  Diamond  kupitia  mtandaoni  na  kumuonesha  mmoja  wa  wacheza  shoo  wa  mwanamuziki  huyo  kuwa  ndo  yeye  Manyota...

Inasemekana  kuwa, pamoja  na  utetezi  wake  huo  ambao  unaweza  kumuingiza  matatani  Diamond,maofisa  hao  wa  usalama  walishndwa  kumuelewa  na  kumtupa  ndani.....

Mtanzania  huyo  alihitimisha  kwa  kudai  kuwa, kutokana  na  mazingira  yalivyo,ni  vyema  mwanamuzi  Diamond  akawa  makini   sana  kama  atakuwa  na  safari  za  kwenda  China  kwani  kwa  namna  moja  ama  nyingine  jina  lake  limewekwa  kwenye  orodha  ya  majina  machafu   na  wanaweza  kumkamata  kwa  lengo  la  kuujua  ukweli...

NIPO TAYARI KUFA KWA AJILI YA DIAMOND

Stori: Imelda Mtema
DADA wa hiyari wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Halima Kimwana amejichora tatuu ya jina la staa huyo na kudai anampenda na yupo tayari kufa kwa ajili yake.

Alisema ukaribu wake ni wa kawaida lakini yupo tayari kufa badala yake (Diamond).
“Nipo tayari kufa kwa ajili ya Diamond, nimechora tatuu ya jina lake mkononi kuonesha msisitizo, namkubali” alisema Halima.

DALILI ZA MWISHO WA DUN IA

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship (FGBF) lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam, Zakaria Kakobe ameibuka na kuweka wazi kuwa kuonekana kwa Mwezi Mwekundu (Blood Moon),   Aprili 15, mwaka huu ni ishara kuu ya mwisho wa dunia kama maandiko yanavyosema katika Matendo 2:17-21, Uwazi linakumegea kwa kina.
Askofu Kakobe aliyasema hayo juzi kufuatia tukio hilo lililojiri siku tano kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo mwezi wote ulipatwa (lunar eclipse) na kuwa mwekundu kama damu,  tukio ambalo pia litatokea tena mwakani.Kufuatia tukio hilo lenye kuogofya,…
NA WAANDISHI WETU
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship (FGBF) lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam, Zakaria Kakobe ameibuka na kuweka wazi kuwa kuonekana kwa Mwezi Mwekundu (Blood Moon),   Aprili 15, mwaka huu ni ishara kuu ya mwisho wa dunia kama maandiko yanavyosema katika Matendo 2:17-21, Uwazi linakumegea kwa kina.
Askofu Kakobe aliyasema hayo juzi kufuatia tukio hilo lililojiri siku tano kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo mwezi wote ulipatwa (lunar eclipse) na kuwa mwekundu kama damu,  tukio ambalo pia litatokea tena mwakani.Kufuatia tukio hilo lenye kuogofya, baadhi ya mitandao ya kijamii duniani kote imekumbushia maneno ya manabii mbalimbali lakini zaidi kutoka kwenye Biblia wakisema mwisho wa dunia sasa ni dhahiri.
MSIKIE KWA UNDANI
“Kinachotakiwa kwa watu sasa ni kuacha maovu na kumrudia Mungu. Ni wajibu wa kila mtu kujiweka tayari kwa kuokoka kwani bila kufanya hivyo watakaokutwa katika dhambi watatupwa jehanamu,” alitahadharisha  Askofu Kakobe.
Aliongeza kuwa, dalili zote za mwisho wa dunia zilizotajwa katika Biblia ziko wazi kwa sasa, kama vile hilo la mwezi wa damu, kuzuka kwa manabii wa uongo, vita ya nchi na nchi na ukoo kwa ukoo lakini akasema  hajui ni kwa nini watu hawataki kuokoka.
NAYE MAMA RWAKATARE
Naye Mchugaji wa Kanisa la Assemblies of God ‘Mikocheni B’ la jijini Dar, Mama Getrude Rwakatare alikiri kulijua hilo la mwezi kuwa wa damu na kusema katiba Biblia, Luka  21:25 Mungu amefafanua kuwa kuna dalili mbalimbali zitajitokeza siku za mwisho wa dunia na sasa zinaanza kuonekana, akawataka watu kuomba bila kuchoka.
“Dalili nyingine ni mataifa kupigana, upendo wa wengi kupoa, manabii wa uongo kuibuka na kadhalika. Haya tunayaona sasa, hivyo watu wote tumrudie Mungu,” alisema Mama Rwakatare.
NABII SUGUYE PIA
Uwazi lilibahatika kuzungumza na Nabii Nicolaus Suguye wa Kanisa la Huduma na Neno la Upatanisho ambaye alisema dalili za mwisho wa dunia ni nyingi ambazo ni mataifa kupigana, kukosa uhusiano mzuri na kuzuka kwa manabii  wa uongo.
NABII GEODAVIE AJUAVYO YEYE
Uwazi lilikwenda mbele zaidi kwa kuzungumza na kiongozi wa Kanisa  la Ngurumo za Upako lenye makao makuu jijini Arusha, George David ‘GeoDavie’ ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Suala la kupatwa  kwa  mwezi  na kuwa  damu  ni ishara ya mwisho wa dunia lakini nasisitiza kuwa pia ni jambo la kisayansi zaidi.”
Alizidi kusema kuwa kilichoandikwa kwenye Biblia, Luka  21:25 (Tena kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota na katika nchi, dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake) lazima kikubalike na kila anayemwamini Mungu.
IMANI MWAKYOMA WA TAG
Mchungaji Imani  Mwakyoma wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Magomeni jijini Dar, yeye alisema kupatwa kwa mwezi na kuonekana wa rangi ya damu ni mafundisho ambayo watumishi wa Mungu wamekuwa wakiihubiri kila kukicha.
“Tumekuwa  tukihubiri kwa muda wa miaka kumi sasa kwamba mwisho utafika pale tu ishara ya anga itakapoanza kuonekana, mwezi kuwa wa damu na jua kuwa giza, siku hizi kila mara jua linapatwa na kuwa giza, bado nini sasa hapo? Watu wamrejee Mungu,” alisema Mchungaji Mwakyoma.
ASKOFU MALASUSA, KARDINALI PENGO
Baadhi ya waumini wa kanisa la Romani Katoliki linaloongozwa na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo na Kanisa la KKT linaloongozwa na Askofu Dr. Alex Gerhaz Malasusa, walisema watumishi hao wa Mungu mara kwa mara wamekuwa wakihubiri watu kutubu kwa kuwa siku za mwisho wa dunia zipo dhahiri kwa sasa.

MCHUNGAJI WA MAREKANI
Naye John Hagee, Mchungaji wa Kanisa la Cornerstone, San Antonio, Texas Marekani na mwanzilishi wa muunganiko wa Wakristo nchini Israeli alishawahi kutoa kitabu akiongozwa na taasisi ya uchunguzi wa anga za juu ya nchi hiyo, NASA kwa kufanya makadirio kupitia historia ambapo aliandika uhusiano wa moja kwa moja kati ya kupatwa kwa mwezi na kuwa mwekundu na utabiri wa Waisrael na wanadamu wote.
NI KARIBU NA PASAKA TU?
Katika kitabu hicho, Mchungaji Hagee aliandika kwamba, zaidi ya miaka 500 iliyopita kupatwa kwa mwezi wa damu kulitokea siku ya kwanza ya Sikukuu ya Pasaka mara tatu tofauti.'
Hata Aprili mwaka huu, mwezi huo ulipatwa na kuwa mwekundu kuelekea Sikukuu ya Pasaka na itatokea tena mwakani kipindi cha Pasaka.
LAZIMA WATU WAJUE ISHARA
Mchungaji Hagee alifafanua kwamba kupatwa kwa mwezi ni lazima watu, hasa Wakristo waelewe ishara hizo.  Alisema katika Biblia, Joel: 2 na Matendo ya Mitume: 2 vyote vimeandika tukio hilo kwamba ndiyo mapito ya dunia kuelekea mwisho wake.
BAADA YA MATUKIO HAYA
Kwa mujibu wa Markell, mchambuzi wa mambo ya sayansi, kupatwa kwa mwezi na kuwa wa damu kutatokea tena katika mpangilio wa Oktoba 8, 2014, Aprili 4, 2015 na Septemba 28, 2015!
IMANI YA KIKRISTO
Hata hivyo, Markell anasema kuwa Wakristo wengi wanaamini maneno ya kale kwamba kupatwa kwa mwezi ni dalili ya ujio wa pili wa Kristo na hivyo kusababisha hofu miongoni mwa wale ambao hawajui maana halisi japo maelezo ya kisayansi yanafafanua jambo hili.
Alisema kimsingi, rangi ya mwezi ni nyekundu ambayo ipo katika anga ya dunia na kama dunia haina anga, moja kwa moja mwezi utafunikwa na giza.
Markell ambaye anaamini kwamba shetani yupo nyuma ya harakati za maendeleo, anasema hakuna mtu anayejua ishara za mwezi lakini alipendekeza kuwa dunia inapaswa kubashiri kwa habari mbaya.

<<<<GPL>>>>

Tuesday, 22 April 2014

CHADEMA YAENDELEA KUSAMBARATIKA

Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki




Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru wadhifa huo kuanzia Aprili mwaka huu kutokana na mkanganyiko wa uongozi ndani ya chama hicho.

Mwapiki amesema amechoshwa na marumbano ya mara kwa mara na meza kuu ndani ya chama hicho katika ngazi ya wilaya hivyo kudhoofisha juhudi zake za kukijenga chama hicho.

Aidha Mwampiki amesema viongozi wa chama hicho wamekuwa na marumbano ya mara kwa mara hivyo yeye kama kiongozi hayupo tayari kuona mambo yanavurugika katika chama hicho.

Hata hivyo katika uamuzi aliouchukua Lucas Mwapiki amesema kuwa yeye atabakia kuwa mwanachama wa chama hicho na Diwani wa Kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

Amewataka wanachama wamuelewe hivyo ameona yeye akae pembeni badala ya kuwa na muda mwingi wa kujadili migogoro ambayo haina tija na kuleta mkanganyiko kwa wanachama.

LIGI YA WILAYA YA MKINGA YAPAMBA MOTO

 Mkuu wa wilaya ya mkinga wakwanza mbele akikagua timu ya shikashika kasbla ya ligi ya walaya kuanza wa pili ni afisa tarafa wa tarafa ya mkinga na watatu ni mdhamini  wa ligi hiyo ndugu Saidi Mbaruku


Kikosi cha SHIKASHIKA FC  kabla ya mechi ya ligi ya wilaya ya mkinga


Kocha Mkuu wa SHIKASHIKA FC ndugu ALEX MWANGA "FERGASON" akitoa maelekezo kwa wachezaji wake kabla ya mechi ya ligi ya wilaya mkinga

Mkuu wa wilaya wakiendelea kufuatilia mechi hiya kati ya SHIKASHIKA FC NA CHUI FC hatimaye mechi hiyo iliisha chui fc 2 ,shikashika 1