Saturday, 6 December 2014

CHRISTIAN KUFUNIKA DAR

Stori: Showbiz
WAKATI siku zikizidi kukatika kuelekea Desemba 6, katika ule Usiku wa Nani Kama Mama ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem, jijini Dar ambapo Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’ anatarajiwa kuweka historia mpya ndani ya ukumbi huo.
Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’.
Akipiga stori na Showbiz, Meneja wa Bella, Amiri Marusu aliongelea usiku huo ambao umekuwa gumzo kubwa kwakuwa ni mara ya kwanza kufanyika uzinduzi wa Albamu ya Nani Kama Mama ndani ya Dar Live hivyo Bella amejipanga vya kutosha kwa kuweka historia mpya ukumbini hapo. “Mashabiki wakae mkao wa kusikia ngoma kali zote kama vile Hanitaki Tena, Usilie aliyoimba na Banana Zoro, Msaliti, Nakuhitaji na nyingine kibao ambazo zipo katika albamu hiyo,” alisema Amiri.
Christian Bella ‘Obama’ akipozi.
Bella ambaye alitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kutua katika bendi ya Akudo Impact na kutengeneza ngoma kali kama Walimwengu si Wanadamu, Bomoa Bomoa, Safari Sio Kifo, Yako Wapi Mapenzi na nyingine nyingi. Ametokea kujizolea umaarufu kwa sauti nyingi tofauti kiasi cha kupelekea kutungiwa jina la Mfalme wa Masauti.

No comments:

Post a Comment