Tuesday, 24 February 2015

MAPIGANO YA TANGA KUMBE WALIKUWA NI MAKOMANDO

                
Na Waandishi Wetu/Uwazi

YALE mapigano yaliyotikisa Mapango ya Amboni jijini Tanga kwa saa 48 kati ya watu wanaodaiwa na wananchi kuwa ni magaidi na majeshi ya ulinzi ya Tanzania bado ngoma nzito kufuatia baadhi ya wananchi kusema mengine mapya wanayoyajua kuhusu magaidi hao, Uwazi limechimba na kuchimbua.

Polisi wakipambana na magaidi hao.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi wa Vijiji vya Mafuriko, Mikocheni, Majimoto, Kilomoni na Amboni yenyewe, wanaamini wahalifu hao ni makomandoo wazuri na waliishi kwenye…


 YALE mapigano yaliyotikisa Mapango ya Amboni jijini Tanga kwa saa 48 kati ya watu wanaodaiwa na wananchi kuwa ni magaidi na majeshi ya ulinzi ya Tanzania bado ngoma nzito kufuatia baadhi ya wananchi kusema mengine mapya wanayoyajua kuhusu magaidi hao, Uwazi limechimba na kuchimbua.

Polisi wakipambana na magaidi hao.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi wa Vijiji vya Mafuriko, Mikocheni, Majimoto, Kilomoni na Amboni yenyewe, wanaamini wahalifu hao ni makomandoo wazuri na waliishi kwenye mapango hayo wakijua siku wakivamiwa watapambana vikali.
KWA NINI MAKOMANDOO?
Mkazi mmoja wa Kijiji cha Majimoto alisema kwa jinsi watu hao walivyofanikiwa kutoweka katika mazingira tata huku wakiwa salama haingii akilini kwamba ni wapiganaji wenye mafunzo ya kawaida.
“Wakati risasi zinapigwa na serikali inatuambia tuchukue tahadhari kwa mtu tusiyemjua tumtolee taarifa tuliamini lazima watakamatwa hata kama si wote. Lakini tulipoambia hali imetulia lakini hajakamatwa hata mmoja tulishangaa sana,” alisema mkazi huyo akiomba asitaje jina lake.

KUMBE WAPO TANGU 2013!
Akizungumza na Uwazi, mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Amboni aliyejitambulisha kwa jina moja la Hassan alisema magaidi hao walipiga kambi kwenye mapango hayo tangu mwaka 2013.
“Sisi tulianza kuwaona mwaka 2013, sikumbuki mwezi. Lakini walionekana kama wachimba kokoto ndiyo maana walidumu kwa muda wote huo. Pale kuna sehemu watu wanachimba kokoto.”

ILIKUWA KAMA KWAO
“Naweza kusema walipatawala pale kwani ilikuwa kukicha, wengine walikuwa wakienda mjini wengine wanashinda palepale. Haikuwa rahisi kudhani ni magaidi,” alisema Hassan.

MAMBO MATATU YAIBUKA
Hata hivyo, wananchi hao ambao wanasema mpaka sasa hawana amani licha ya kuwepo kwa askari polisi kila kona kulinda, walisema kuna mambo matano ambayo polisi wamekaa kimya kuyatolea ufafanuzi.


Polisi wakiwa kwenye mapambano.
MOSI
“Sisi wakazi wa hapa palipotokea mapigano tunajiuliza, kwa nini polisi wameshindwa kutuambia ukweli wale ni akina nani badala ya kusema majambazi.

“Tangu lini majambazi wanapiga kambi mahali? Mimi ninavyojua, majambazi hufanya uhalifu na kurudi makwao. Tena naamini majambazi tunapanga nao nyumba tunazoishi au tunaishi nao mtaa mmoja au jirani,” alisema Almasi, mkazi wa Kijiji cha Kilomoni.
PILI
Wakazi hao walikwenda mbele zaidi na kusema kuwa, tangu Tanzania ipate uhuru haikuwahi kutokea majambazi wakapambana na polisi halafu polisi wakashindwa hadi kuita wanajeshi na wasikamatwe hata mmoja?

TATU
Wakazi hao waliendelea kudai kuwa, wamesikia tetesi zinazodai mwanajeshi aliyeuawa yalitokea makosa ya kiufundi kutoka kwa majeshi yetu lakini wanashangaa kimya cha polisi licha ya habari hizo kusambaa sana Amboni.

“Sisi tunasikia yule askari aliyeuawa ilitokana na makosa ya kiufundi kutoka kwa wenzake. Watu wengi hapa Mafuriko wanasema wamesikia hivyo, jeshi lingekanusha au kufafanua kama kuna ukweli,” alisema Mgaya, mkazi wa kijiji hicho.
WANANCHI MAPEMA NDANI
Baadhi ya wakazi walizungumza na Uwazi walisema licha ya kuwepo kwa polisi maeneo hayo lakini wanalazimika kuingia ndani mapema kwani kuna minong’ono kuwa, wahalifu hao wamejipanga kurudi na nguvu mpya baada ya kwenda kukutana na wenzao kwenye nchi jirani lakini jeshi la polisi mkoani hapa limekanusha uvumi huo na kuwataka wananchi waendelee na shunguli zao za kila siku.


Magaidi wa Al-Shabaab.
AL- SHABAAB ALIYEKIMBILIA KANISANI DAR...
Wakati huohuo, kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Shaban, mwenyeji wa Iringa ambaye alikiri kanisani kupewa mafunzo ya kigaidi nchini Afghanistan ili kwenda kutumika na Kundi la Al-Shabaab nchini Somalia ametoweka.

Akizungumza na Uwazi, Mchungaji wa Kanisa la Victoria lililopo External-Ubungo jijini Dar, John Said alisema Shaban alifika kanisani kwake mwaka jana na kutoa ushuhuda mzito kwamba yeye na Watanzania wenzake wawili walipelekwa Afghanistan kwa ajili ya mafunzo ya dini lakini walipofika wakakuta  ni mafunzo ya kigaidi.
“Shaban alitoweka, haji tena kanisani kama zamani. Alipokuja kwa mara ya kwanza alitoa ushuhuda huo mzito lakini baadaye akakata mguu,” alisema mchungaji huyo.
Katika ushuhuda wake, Shaban alisema kuwa, baada ya kufuzu walipelekwa Somalia kuungana na Al-Shabaab na kupigana na majeshi ya serikali ya nchi hiyo kwa kutumia silaha nzito lakini mwishowe aliamua kutoroka kurudi nchini.



Anasema: “Siku moja katika mapambano na majeshi ya serikali nilishuhudia wale wenzangu wawili wakiuawa kwa risasi, mimi nikatoroka katika eneo la mapigano kwa kuruka ukuta, ndiyo nikarudi hapa nyumbani Tanzania.”
UWAZI LAZUNGUMZA NA CHAGONJA
Baaada ya gazeti hili kuchimba yote hayo, lilimtafuta Kamishna wa Oparesheni ya Mafunzo Jeshi la Polisi Tanzania, Paul Chagonja ambapo alipopatikana na kumsimulia mambo yote mpaka ya Shaban, alisema:

“Mimi niko nje ya nchi kwa kazi ya kitaifa, wasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (Juma Ndaki) akupe maendeleo ya oparesheni yetu kule.

“Kuhusu huyo Shaban, nawasiliana na kitengo cha intelejensia sasa hivi ili atafutwe mpaka apatikane. Si yeye tu msako mkali unaendelea kwa umakini juu ya watu hao.”Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga alipotafutwa juzi, simu yake ilikuwa hewani lakini hali ya hewa ilikuwa mbaya hivyo kukosa usikivu.

BY GPL>>>>>>>>>>>>>

MAZISHI YA MEZ B

                
IMG-20150223-WA0040
Wananchi wakiwa wamebeba  mwili wa marehemu Marehemu Mez B baada ya kuagwa na mashabiki wa mziki pamoja na ndugu jamaa na marafiki mwili wake ulielekea kupumzishwa katika makaburi ya Wahanga Maili mbili jana.
IMG-20150223-WA0036
Mama mzazi wa Mez B, Marry Mkandawile (katikati) akiwa ameshikiliwa na ndugu baada ya kuingia viwanja vya Mashujaa ili kutoa heshima za…

IMG-20150223-WA0040
Wananchi wakiwa wamebeba  mwili wa marehemu Marehemu Mez B baada ya kuagwa na mashabiki wa mziki pamoja na ndugu jamaa na marafiki mwili wake ulielekea kupumzishwa katika makaburi ya Wahanga Maili mbili jana.
IMG-20150223-WA0036
Mama mzazi wa Mez B, Marry Mkandawile (katikati) akiwa ameshikiliwa na ndugu baada ya kuingia viwanja vya Mashujaa ili kutoa heshima za mwisho.
IMG-20150223-WA0037 IMG-20150223-WA0038
Baadhi ya wasanii waliohudhuria msiba wa Mez B wakiwa kwenye majonzi mazito
IMG-20150223-WA0039  IMG-20150223-WA0041 IMG-20150223-WA0042 IMG-20150223-WA0044
Mtangazi wa Citizen TV anayejulikana kwa jina la Mzazi Willy Tuva akifanya mahojiano na msanii wa Bongo Fleva Janjaro.
(PICHA: DJ CHOKA

Saturday, 6 December 2014

SIMBA INATISHA

SIMBA imefanya usajili mwingine wa kimyakimya baada ya kumsajili mshambuliaji raia wa Gambia.
Mshambuliaji huyo ametajwa kwa jina la Omar Mboob aliyewasili jana usiku kwa Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.
Ingawa viongozi wa Simba hawakuwa wakipokea simu jana, taarifa za uhakika zinaeleza mshambuliaji huyo kinda anatarajia kuanza mazoezi leo na Simba.
“Kweli Simba wamekuja usiku wa jana (juzi) wakampokea mchezaji mmoja na wamesema anatokea Gambia.
“Walikuja na Hiace yao hapa wakampokea na kuondoka naye lakini walifanya mambo yao harakaharaka utafikiri kuna jambo la uficho.“Nilimsikia kiongozi mmoja akitaka waondoke haraka hapa airport kwa kuwa waliwahofia Yanga,” kilieleza chanzo cha uhakika kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa Kamati ya Utendaji ya Simba alipoulizwa jana, alionekana kushangazwa na swali hilo, lakini hakutoa jibu.“Nani kakuambia, mimi sijui lolote. Wamekuambia anatokea nchi gani? Ila ukweli sina habari ndugu yangu,” alisema.
Ila taarifa za uhakika, zinasisitiza mshambuliaji huyo amefichwa na viongozi wa Simba wamekuwa wakifanya siri kubwa kuhakikisha haijulikani.
Lengo ni kuepuka Yanga au klabu nyingine kuingilia kati ili wajaribu kuona kiwango cha mchezaji huyo kutokea katika Jiji la Banjul, Gambia.Iwapo Mgambia huyo atafuzu, basi itakuwa ni hatari kwa Warundi, Amissi Tambwe na Pierre Kwizera kwa kuwa mmoja wao atalazimika kuachia nafasi.SI

CHRISTIAN KUFUNIKA DAR

Stori: Showbiz
WAKATI siku zikizidi kukatika kuelekea Desemba 6, katika ule Usiku wa Nani Kama Mama ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem, jijini Dar ambapo Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’ anatarajiwa kuweka historia mpya ndani ya ukumbi huo.
Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’.
Akipiga stori na Showbiz, Meneja wa Bella, Amiri Marusu aliongelea usiku huo ambao umekuwa gumzo kubwa kwakuwa ni mara ya kwanza kufanyika uzinduzi wa Albamu ya Nani Kama Mama ndani ya Dar Live hivyo Bella amejipanga vya kutosha kwa kuweka historia mpya ukumbini hapo. “Mashabiki wakae mkao wa kusikia ngoma kali zote kama vile Hanitaki Tena, Usilie aliyoimba na Banana Zoro, Msaliti, Nakuhitaji na nyingine kibao ambazo zipo katika albamu hiyo,” alisema Amiri.
Christian Bella ‘Obama’ akipozi.
Bella ambaye alitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kutua katika bendi ya Akudo Impact na kutengeneza ngoma kali kama Walimwengu si Wanadamu, Bomoa Bomoa, Safari Sio Kifo, Yako Wapi Mapenzi na nyingine nyingi. Ametokea kujizolea umaarufu kwa sauti nyingi tofauti kiasi cha kupelekea kutungiwa jina la Mfalme wa Masauti.

Saturday, 11 October 2014

JEMBE KINANA AENDELEA KUVUNJA CHADEMA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akionesha kadi 27 za wananchama wa Chadema  waliokihama chama hicho na kujiunga na CCM kaatika mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Nyololo, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010. Kulia aliyevaa shati jeupe ni aliyekuwa Katibu wa Kata ya Igowole, Josephat Soda ambapo wengine ni miongoni mwa walio kuwa wafuasi wa Chadema.
 Aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Igowole, Joephat Soda akikabidhi bendera ya chama hicho kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya yeye na wenzie 26 kutangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo.
 Kinana akimkabidhi kadi ya CCM, Josephat Soda baada ya kutanga kujiunga na CCM katika mkutano huo.
 Josephat Soda akielezea jinsi alivyoamua kuondoka Chadema na kujiunga na CCM, ambapo alisema amechoka na chama kilichosheheni uongo, ambapo viongozi wa Chadema alidai kuwa walitoa maagizo kuwaakope fedha za  kujengea Mnara wa mwandishi wa habari Marehemu David Mwangosi, aliyeuawa wakati wa vurugu za Chadema na Polisi katika Mji wa Nyololo, ambapo walimuahidi kumtumia fedha zilizotumika kujenga mnara huo ahadi ambayo hadi sasa haalipwa na anadaiwa na muuza simenti na muuza saruji alikokopa. CCM imeamua kulipa madeni yote aliyokuwa akidaiwa.
Wanachama wa CCM wakiwemo wapya kutoka Chadema, wakiapa kiapo cha utii cha CCM baada ya kukabidhiwa kadi wakati wa mkutano huo.
<<<<<<<<GPL>>>>>>>>

JAMBAZI SUGU LAUWAWA ARUSHA

 
Wakazi wa Jiji la Arusha wakiwa katika Kituo cha Polisi mkoani humo kushuhudia mwili wa mtu anayedaiwa kuwa jambazi sugu, Ramadhan Abdallah Jumanne (Rama Ndonga), aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi usiku wa kuamkia jana. Picha na Happy Lazaro.       


Arusha. Jeshi la Polisi mkoani Arusha limefanikiwa kumuua jambazi aliyekuwa akiutikisa mkoa huo kwa matukio ya kuteka na kuwapora wanawake wenye magari na kisha kuwapiga risasi.
Mtu huyo aliyefahamika kwa kwa jina la Ramadhan Abdallah Jumanne maarufu kama Rama Ndonga (37) Mkazi wa Moivo hatimaye ameuawa polisi baada ya kupigwa risasi katika majibizano na askari wa jeshi hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema jambazi huyo aliuawa usiku wa kuamkia jana majira ya saa 2:04 usiku katika Kijiji cha Moivo, Kitongoji cha Enaboishu wilayani Arumeru.
Alisema baadhi ya matukio ya ujambazi aliyowahi kuhusika nayo ni lililotokea Agosti 6 mwaka huu saa 3:30 usiku maeneo ya Kwa Iddi ambapo walimpiga risasi sehemu ya shingo mwanamke Shamimu Rashid aliyekuwa Mkazi wa Sakini wakati akijiandaa kuingia nyumbani kwake na kumuua.
Kamanda Sabas alitaja tukio lingine ni la Agosti 21 mwaka huu majira ya saa 1:00 huko maeneo ya Olasiti, jambazi huyo akiwa na mwenzake kwenye pikipiki walimjeruhi kwa kumpiga risasi ya mdomoni na kutokea kichwani mtoto Christen Nickson mwenye umri wa miaka mitatu na nusu na kisha kufanikiwa kupora Sh200,000 na baadaye majeruhi huyo alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru.
Aidha, kukamatwa kwa jambazi huyo ni baada ya polisi kutumia mbinu za kisasa na kufika nyumbani kwa marehemu na polisi walimwamuru ajisalimishe lakini alikaidi na kuanza kuwarushia risasi hali iliyosababisha askari kujibu mapigo na hatimaye kusababisha kifo chake.
Alisema kuwa, baada ya upekuzi mwili wa marehemu ulipatikana na bastola aina ya Glock 19 yenye namba RLU 976 iliyotengenezwa nchini Australia ikiwa na magazine yenye risasi 14 ambayo alikuwa ameishika mkononi pamoja na maganda matano ya risasi.
Aidha, upekuzi zaidi uliofanywa katika chumba chake ulibaini magazine moja yenye risasi 15 na magazine mbili zenye uwezo wa kubeba risasi 30 kila moja, redio call moja yenye nembo ya ITSS/UNICTR, pikipiki aina ya Toyo Power King rangi nyekundu yenye namba za usajili T 507 BSU.
Upekuzi zaidi ulibaini kofia ngumu ya kuendesha pikipiki rangi nyekundu, plate number ya pikipiki yenye namba T 805 CVD, pingu moja, Glock Fab Defence moja na vifaa vya kusafishia bastola pamoja na koti jeusi.
Kamanda Sabas alisema polisi wanaendelea kumsaka mwenzake waliyekuwa wakitumia naye pikipiki hiyo, ili kuweza kuutokomeza mtandao huo ambao umekuwa tishio jijini Arusha.
Kutokana na tukio hilo, watu walifurika kituo cha polisi kushuhudia mwili wa marehemu ambaye aliutikisa mji huo.

POLICE 120 WATIMULIWA CHUONI MOSHI

 
Moshi. Maofisa wa Polisi wapatao 120 wa Jeshi la Polisi, waliokuwa wakihudhuria mafunzo ya kupandishwa vyeo katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA), wametimuliwa chuoni hapo.
Habari za uhakika zilizopatikana jana kutoka ndani ya chuo hicho zamani kikijulikana kama CCP, zimedai uamuzi wa kuwaondoa chuoni ulitangazwa jana na mkuu wa chuo hicho, Matanga Mbushi.
Vyanzo mbalimbali vililidokeza gazeti hili kuwa, waliotimuliwa chuoni hapo ni maofisa ambao wana ulemavu wa aina mbalimbali walioupata wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi.
Habari hizo zilisema hadi jana saa 9:00 alasiri, maofisa hao walikuwa ofisi za mkuu wa chuo hicho wakisubiri kupatiwa maelekezo ya namna ya kurejea katika vituo vyao vya kazi mikoa mbalimbali.
“Wako 120 hivi walikuja hapa (MPA) kwa ajili ya kuchukua kozi za Koplo, Sajenti, Meja na ‘Assistant Inspector’ (wakaguzi wasaidizi), lakini ndiyo hivyo wametuambia tuondoke,” kilidokeza chanzo chetu.
Hata hivyo, ofisa mmoja alilidokeza gazeti hili kwamba mkuu wa zamani Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, ambaye amestaafu, ndiye wa kulaumiwa kwa kutoheshimu mapendekezo ya wataalamu.
“Tulimwambia IGP Mwema kwamba ni vizuri kama maofisa wenye ulemavu kama baadhi ya vigezo wanavyo basi wapewe vyeo huko huko mikoani, lakini wasiende chuoni,” alidokeza na kuongeza;
“Tulipendekeza yafunguliwe madarasa ya kanda wakishafanya mtihani wa kawaida wapewe vyeo huko huko, lakini wakija chuoni ni lazima wahudhurie vipindi vyote ambavyo vinafanya chuo kiitwe chuo.
“Chuo chochote kile kina vigezo vyake na kwamba ili mtu apate cheo alichokwenda kukisomea ni lazima ahudhurie asimilia 95 ya vipindi ikiwamo kwata, medani za kivita na kuzuia vurugu,”alisema.
Chanzo kingine kililidokeza gazeti hili kuwa maofisa hao waliripoti chuoni hapo wiki mbili zilizopita na katika uchunguzi, walibainika wana ulemavu ambao hawawezi kumudu mafunzo ya ukakamavu.
Mmoja wa maofisa hao waliotimuliwa alilalamika kuwa kitendo hicho siyo cha kiungwana kwa kuwa ulemavu huo waliupata wakiwa kazini wakilitumikia Taifa na hawajashindwa kuingia darasani.
“Baadhi yetu tumefanya kazi miaka 20 wengine 25. Wamekatika miguu. Wako trafiki wamegongwa na polisi wengine wamepigwa risasi na majambazi wakapata ulemavu si sawa kutunyima vyeo,”